Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, February 25, 2015

FAINALI KOMBE LA DUNIA 2022 – QATAR: JOPO LA FIFA LAPENDEKEZA KUFANYIKA NOVEMBA, DESEMBA KUEPUKA JOTO

KIKOSIKAZI cha FIFA kimependekeza kuwa Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2022 zitakazochezwa Nchini Qatar zichezwe Mwezi Novemba na Desemba.
Sambamba na hilo, pia imependekezwa kuwa Fainali hizo zifupishwe kwa sababu ya kuziondoa muda wake wa kawaida wa Miezi ya Juni na Julai.
Sababu kubwa ya Fainali hizo za Mwaka 2022 kupendekezwa kutochezwa Juni na Julai ni kutokana na hali ya joto ambalo hufikia zaidi ya Nyuzijoto Sentigredi 40 huko Qatar katika kipindi hicho.
Baada ya Qatar kuteuliwa kuwa Mwenyeji wa Fainali za 2022 kuliibuka upinzani mkubwa kuhusu uamuzi huo huku ikitajwa Joto kuwa kipingamizi licha ya Nchi hiyo kusema iko tayari kutumia Teknolojia kwenye Viwanja ili kupoza hali ya Hewa.

Ndipo FIFA ilipoamua kuweka Kikosikazi ili kushauriana na Watangazaji, Wadhamini, Wadau wengine na hasa Ligi kubwa za Soka Barani Ulaya.

Kufuatia mashauriano ya Miezi 6 Kikosikazi hicho kimetoa Mapendekezo yao baada ya Mkutano wao huko Doha, Qatar hii Leo.

Kamati Kuu ya FIFA, itakayokutana huko Zurich, Uswsisi hapo Machi 19 na 20 ndio itatoa uamuzi wa mwisho.

No comments:

Post a Comment