Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, September 12, 2014

TUZO ZA MWEZI LIGI KUU ENGLAND, WAGOMBEA WATAJWA YUMO KOCHA MOURINHO, COSTA NA FABREGAS

WADHAMINI wa Ligi Kuu England wametangaza Listi ya Wagombea wa Tuzo za Mwezi za Meneja Bora na Mchezaji Bora na miongoni mwao ni Jose Mourinho, Meneja wa Chelsea, huku Wachezaji wake Diego Costa na Cesc Fabregas wakiwemo.
Kwa upande wa Mameneja yupo pia yule wa Swansea City Garry Monk ambae ameiongoza Timu yake kushinda Mechi zao zote 3 za kwanza za Ligi na pia yuko Meneja wa Stoke City Mark Hughes ambae Timu yake iliwafunga Mabingwa Manchester City katika Mechi iliyopita huko Etihad.

Pia yupo Paul Lambert wa Aston Villa ambae Timu yake imeshinda Mechi mbili na Sare moja.
Kwa upande wa Wachezaji yuko Straika wa Chelsea Diego Costa ambae ameifungia Timu yake Bao katika kila Mechi ya Ligi waliyocheza na pia yumo Kiungo wa Timu hiyo Cesc Fabregas ambae amekuwa aking’ara katika Mechi zote.

Wengine ni Nathan Dyer wa Swansea ambae amepiga Bao 3 na pia yuko Mchezaji mwenzake wa Timu hiyo Gylfi Sigurdsson.
Wa mwisho kwenye Listi ya Wagombea kwa Wachezaji ni Mchezaji wa Aston Villa
Andreas Weimann ambae ameifungia Timu yake Mabao ya ushindi dhidi ya Stoke na Hull City

No comments:

Post a Comment