Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, August 8, 2017

OKWI NA NIYONZIMA WANOGESHA PILAU LA SIMBA DAY




WACHEZAJI wapya wa Simba, Emmanuel Okwi na Niyonzima  wamewapagaisha mashabiki wakati timu hiyo ikiibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Rayon Sports ya Rwanda.
Mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ulikuwa maalumu kwa ajili ya kuadhimisha Simba Day, ambayo kilele chake kilikuwa leo.
Bao hilo pekee lililonogesha pilau la Simba, liliwekwa kimiani na Mohammed Ibrahim katika dakika ya 16 kufuatia kazi nzuri iliyofanywa na John Bocco 'Adebayoy'.
Mashabiki walilipuka kwa shangwe pale Okwi na Haruna Niyonzima walipotambulishwa rasmi mbele ya mashabiki wa timu hiyo uwanjani hapo.
Mbali na kuwatambulisha wachezaji wao wapya, Simba pia ilitoa tuzo kwa mchezaji wake wa zamani, Abadallah Kibadeni kwa kuisaidia timu hiyo kuifunga Yanga kwa mabao 6-0 baada ya kufunga bao tatu peke yake (hat-trick) mwaka 1977.
Pia Kibadeni alipewa tuzo hiyo baada ya kuisaidia timu hiyo kucheza fainali ya Kombe la CAF mwaka 1993.
Mohammed Hussein `Tshabalala’ amepewa tuzo ya mchezaji bora wa msimu uliopita aliyechaguliwa na mashabiki wa timu hiyo.
Simba iliuanza mchezo huo kwa nguvu, ambapo Okwi nusura afunge katika dakika ya 11, lakini kipa wa Rayon aliupangua mpira.
Simba kila mwaka imekuwa ikiandaa tamasha la Simba Day, ambalo wamekuwa wakilitumia kuwatambulisha wachezaji wao wapya na jezi zao mpya zitakazotumika msimu ujayo nyumbani na ugenini.
Kikosi cha Simba;
Aishi Manula, Erasto Nyoni, Jamal Mwambeleko, Method Mwanjali, Salum Mbonde/Yussuf Mlipili, James Kotei/Jonas Mkude, Shiza Kichuya/Said Ndemla, Muzamir Yasin, Mohamed Ibrahim/Haruna Niyonzima, Emmanuel Okwi/Nicolaus Gyan na  John Bocco `Adebayor’/Laudit Mavugo.

No comments:

Post a Comment