Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, September 18, 2014

PAZIA LA LIGI KUFUNGULIWA JUMAMOSI WAAMUZI WATAKAOCHEZESHA HADHARANI



IKIWA imebaki siku moja kufunguliwa kwa pazia la Ligi Kuu Tanzania Bara, mambo tayari yamenoga baada ya kukamilika kwa safu ya waamuzi watakaochezesha michuano hiyo Jumamosi na Jumapili.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi Tanzania Silas Mwakibinga aliliambia gazeti hili jana, orodha ya waamuzi iko tayari na kuwataka baadhi yao watakaochezesha katika mchezo huo kutenda haki.
Katika mchezo wa Yanga dhidi ya Mtibwa Sugar ya pale Morogoro,  mechi itakayopigwa kwenye uwanja wa Jamhuri itachezeshwa na mwamuzi Dominick Nyamisano kutoka mkoani Dodoma.
Wakati huo, wanalambalamba Azam FC itakuwa mwenyeji wa Polisi ya Morogoro kwenye uwanja wa Azam Complex Chamazi, katika mchezo utakaochezeshwa na Mwamuzi Abdallah Kambuzi kutoka mkoani Shinyanga.
Mchezo mwingine utakaopigwa kwenye uwanja wa Kambarage mkoani Shinyanga kati ya Ndanda Fc dhidi ya wenyeji wa mji Stand United itachezeshwa na Hashim Abdallah wa Dar es Salaam.
Mchezo mwingine utakuwa ni kati ya Mgambo dhidi ya Kagera Suger mchezo utakaopigwa kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga na kuchezeshwa na Mwamuzi Kennedy Mapunda.
Aidha, Ruvu Shooting itacheza na Tanzania Prisons kwenye uwanja wa Mabatini, Mlandizi na kuchezeshwa na Mwamuzi David Paulo wa Mtwara.
Wakati huo, Mbeya City ikiwakaribisha JKT Ruvu kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya katika mchezo utakaochezeshwa na Mohamed Theophil.
Baada ya mchezo huo wa Jumamosi, katika mchezo wa Jumapili watoto wa Msimbazi Simba watakuwa ni wenyeji wa Coastal Union kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mchezo huo utachezeshwa na mwamuzi Jacob Adongo mkazi wa mkoa wa Mara.
Mwakibinga alisema anategemea waamuzi hao watachezesha mchezo huo kwa kufuata  sheria 17 za soka, bila kupendelea na kwa haki.
“Hiyo ndio orodha ya kwanza, kuna nyingine itatoka kwani wapo wengi, na wasaidizi wao tayari, tuna imani watazingatia maadili ya kazi yao,”alisema Mwakibinga.

No comments:

Post a Comment