Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, July 24, 2014

PATRICK VIEIRA AKATAA UBAGUZI, AVUNJA MCHEZO WA VIJANA WA MANCHESTER CITY U-21 HUKO CROATIA

Manchester City wamevunja Mechi yao ya Vijana wa chini ya Miaka 21, U-21, dhidi ya HNK Rijeka huko Novigrad, Croatia hapo Jana kwa madai ya kukashifiwa Kibaguzi kwa mmoja wa Wachezaji wao.
Wakati Mechi ikivunjika, City walikuwa mbele kwa Bao 1-0 na walitoka nje mara tu baada ya Kiungo wao, Seko Fofana, kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu baada kumtandika Teke mpinzani lakini inaaminika hiyo ni sababu ya kukashifiwa.
Lakini kila upande umetoa taarifa tofauti kwa Man City kudai kuwa katika Kipindi cha Kwanza Uongozi wao ulilazimika kuitoa nje Timu yao kufuatia kukashifiwa Kibaguzi kwa Mchezaji wao anaeaminika kuwa ni Seko Fofana, Raia wa France.

Timu ya HNK Rijeka imedai kuwa Kocha wa Man City, Patrick Vieira, aliingia Uwanjani na kuongea na Refa na, kwa mshangao wa wengi, kuamua kuitoa nje Timu yake bila wao kujua ni kwa sababu gani.

Fofana, ambae huchezea France U-19, alijiunga na City Januari 2013 akitokea Klabu ya Ligue 1 huko France, FC Lorient.

Januari 2013, AC Milan walivunja Mechi yao ya Kirafiki dhidi ya Timu ya Daraja la chini huko Italy, Pro Patria, baada ya Mashabiki kumpigia kelele za Kibaguzi Mchezaji wao Kevin-Prince Boateng ambae aliukamata Mpira na kuubutua kwa Mashabiki hao na kisha kuongoza Timu yake kutoka nje na Mechi kuvunjika.

No comments:

Post a Comment