Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, May 10, 2014

NIGERIA YATANGAZA KIKOSI CHA AWALI CHA WACHEZAJI 30 KOMBE LA DUNIA

Kocha wa Nigeria, Stephen Kheshi
SHIRIKISHO la Soka Nigeria (NFF) limetangaza kikosi cha cha awali cha wachezaji 30 kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia la FIFA nchini Brazil baadaye mwaka huu. Kutangazwa kwa wachezaji hao jana, kumefutia kikao cha pamoja baina ya NFF na kocha wa Super Eagles, Stephen Keshi.


Kikosi hicho ni makipa: Vincent Enyeama, Austin Ejide, Chigozie Agbim na Daniel Akpeyi; Mabeki: Elderson Echiejile, Juwon Oshaniwa, Godfrey Oboabona, Azubuike Egwuekwe, Kenneth Omeruo, Joseph Yobo, Kunle Odunlami na Efe Ambrose.

Viungo: John Mikel Obi, Ogenyi Onazi, Ramon Azeez, Joel Obi, Nosa Igiebor, Michael Uchebo, Ejike Uzoenyi, Sunday Mba na Reuben Gabriel, wakati washambuliaji ni: Ahmed Musa, Shola Ameobi, Emmanuel Emenike, Obinna Nsofor, Osaze Odemwingie, Babatunde Michael, Victor Moses, Uche Nwofor na Nnamdi Oduamadi.

Nigeria ni moja kati ya nchi tano za Afrika zitakazoshiriki fainali za Kombe la dunia mwaka huu, pamoja na Algeria, Ghana na Ivory Coast. 

No comments:

Post a Comment