Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, January 20, 2014

ENGLISH PREMIER LEAGUE:EMMANUEL ADEBAYOR AWANYOA SWANSEA, TOTTENHAM 3-1

Swansea City wakicheza leo kwenye uwanja wao Liberty stadium kuwakaribisha Tottenham Hotspurs, Emanuel Adebayor ndie aliyeanza kufungua lango lao Swansea kwa kuwachapa bao safi la kichwa akipewa pasi na  Christian Eriksen katika dakika ya 35 yakipindi cha kwanza. Mwamuzi wa Mtanange huo ni M. Atkinson
Mchezaji wa Swansea Leon Britton akimiliki mpira huku mchezaji wa Tottenham Nacer Chadli akimsikilizia kwa nyuma. Emmanuel Adebayor akijitwisha Bao la kichwa hapa
Emmanuel Adebayor akishangilia bao lake la kwanza alilofungwa kwa kichwa.
Pongezi kwa Emmanuel Adebayor hapa!!!
Kipindi cha pili dakika ya 54 Swansea City wanajifunga bao, Mfungaji wa bao hilo akiwa ni Chico(OG).
Bao la tatu ni la Emmanuel Adebayor tena baada ya kupewa pasi ya mwisho na Danny Rose na hatimaye Adebayor kumfunga kipa wa Swansea City Gerhard Tremmel.
Bao la Swansea City limefungwa na Wilfried Bony katika dakika ya 78 kwa shuti kali. Ushindi huu wa Spurs unawaweka nafasi ya tano wakiwa sawa na Liverpool wakiwa na alama 43 wakitofautiana magoli ya kufunga na kufungwa. Swansea wao wamebakia pale pale nafasi ya 14 wakimsubiria West Brom anayecheza jumatatu usiku na Everton kama atafunga atampita.

VIKOSI:
Swansea City: Tremmel, Rangel, Chico, Williams, Ben Davies, Britton, Amat, Pozuelo, Shelvey (Lamah 51), Routledge, Bony.
Subs: Taylor, Cornell, Tiendalli, Vazquez, Richards, Donnelly.

Booked: Amat, Bony.
Goal: Bony 78.
Tottenham Hotspurs: Lloris, Walker, Dawson, Chiriches, Rose, Bentaleb, Dembele, Lennon (Naughton 79), Eriksen, Chadli (Sigurdsson 67), Adebayor.
Subs: Soldado, Holtby, Capoue, Defoe, Friedel.

Booked: Rose.
Goal: Adebayor 35, 71, Chico og 53.
Referee: Martin Atkinson

No comments:

Post a Comment