Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, January 20, 2014

CHELSEA ILIPOICHAPA MANCHESTER UNITED 3-1, STAMFORD BRIDGE, SAMWEL ETO'O AFUNGA HAT-TRICK

Manchester United walitawala Kipindi cha Kwanza na kujikuta wako nyuma kwa Bao 2-0 dhidi ya Chelsea, Bao zote zikifungwa na Gwiji wa Cameroun Samuel Eto’o, kwenye Mechi ya Ligi Kuu England iliyochezwa Stamford Bridge waliyomaliza kwa kipigo cha Bao 3-1 ambacho kwa Wadau wao huenda kimehakikisha kwamba hawawezi tena kutetea Taji lao kwani sasa wako Pointi 14 nyuma ya Vinara Arsenal huku zimebaki Mechi 16. Manchester United walikuwa Ugenini Stamford kucheza na Chelsea, Chelsea wapo nafasi ya tatu wakati united wakiwa nafasi ya 7 kwenye msimamo wa ligi kuu England. Mwamuzi wa mtanange huu ni - Phil. Dowd‎. Moyes akiingia uwanjani Stamford Bridge

Samuel Eto'o akifunga bao mpira uliotenguliwa na Michael Carrick na hatimaye kuingia langoni mwa United.
Dakika ya 17 Samwel Eto'o anaipatia bao Chelsea na kufanya 1-0 dhidi ya Man united. Bao la pili Samwel akaiongezea tena bao Chelsea katika dakika za mwishoni za kipindi cha kwanza akifunga katika dakika ya 45. Bao la tatu ni la  Eto'o tena..Mchezaji wa Chelsea Ramires akichuana na mchezaji wa United mwenye umri mdogo Adnan Januzaj katika kipindi cha kwanza cha dakika 45. Samuel Eto'o akifunga bao la pili hapa mbele ya Nemanja Vidic na kufanya matokeo kuwa 2-0 Sir Alex Ferguson akiteta na shabiki wa United Mick Hucknall wakati wa mtanange Stamford Bridge usiku huu.
Mzee Ferguson akishuhudia bao 2-0 za Chelsea hapa katikati ya mashabiki.Mmiliki wa timu ya Chelsea nae alikuwepo uwanjani leo StamfordRoy Hodgson nae akishangaa!!
Samwel Eto'o akishangilia moja ya bao zake hapa..
Chelsea walipata Bao lao la kwanza katika Dakika ya 17, bila kutegemewa kwani Man United ndio waliokuwa juu kimchezo, baada ya uzembe wa kutomkaba Samuel Eto'o ambae alipokea Mpira wa kurushwa na kumhadaa kirahisi Phil Jones kisha kupiga Shuti la Mita 20 na kumbabatiza Mchael Carrick na kumpoteza Kipa De Gea.
Bao la Pili lilifungwa kwenye Dakika ya 45 na Eto’o kufuatia ulinzi duni baada Kona kupigwa na kuokolewa na Mpira kumkuta Ramires aliempasia Cahill aliemsogezea Eto’o na kupachika kilaini.

Bao la 3 lilipigwa tena na Eto’o, ni Hetitriki kwake, kufuatia Kona ya Dakika ya 49 iliyounganishwa na Cahill na kuokolewa na De Gea na kutua miguuni mwa Eto’o ambae alimalizia kilaini kwa mara nyingine.

Javier Hernandez ‘Chicharito’ aliifungia Bao lao pekee Man United katika Dakika ya 78 kufuatia kazi njema ya Danny Welbeck kumfikia Phil Jones ambae shuti lake lilionekana kutokuwa na madhara hadi alipochomoza Chicharito.

Man United walimaliza Mechi hii Mtu 10 baada Nahodha wao Nemanja Vidic kupewa Kadi Nyekundu kwa Rafu mbaya kwa Eden Hazard.
David Moyes Kocha wa United akiungalia mpira Mtanange huoDanny Welbeck akiendesha...Samwel Eto'o leo alikuwa mwiba kwa United ndie aliefunga bao zote tatuSamwel Eto'o akifunga bao la kwanza hapa, Bao lililotenguliwa na Carrick na kumwamisha kipa De Gea uelekeo na kuzama nyavuniDavid De Gea ..akifungwa tena hapa na Eto'o
Eto'o akishangilia baada ya kufunga bao la pili hapa.
Majanga: Januzaj na Danny Welbeck wakilianzisha baada ya kufungwa bao na SamwelUnited Hoi....Mashabiki wakitoa ujumbe wao uwanjani stamford Kocha wa Blues Jose (kulia) akitoa maelekezo kwa OscarBao...Nipishe nikashangilie!!
Hot streak: Chelsea players celebrates Eto'o's (right) second goal of the game against United
Wachezaji wa Chelsea wakimpongeza Eto'o
Lone man: Danny Welbeck (right) gets past Ramires during Chelsea's win against United
Danny Welbeck kwenye mbio akikimbia na Ramires William akiendeleza mashambuliziJones leo ameshindwa kumkaba WilliumYoung kidogo amfunge kipa wa ChelseaSamwel katikati akikimbia huku akishangilia baada ya kuwafunga bao la tatu United
Eto'o akipokea pongezi kutoka kwa viongozi wake kwenye benchEto'o  akifanya yake mbele ya Camera!!Gary Cahill  akishangilia...Moyes ...David Beckham hakuwa na furahaRoman Abramovich Petr Cech chupuchupu afungwe na Javier Hernandez...Antonio Valencia...
Javier Hernandez akishangilia bao lake katika dakika ya 78Nemanja Vidic kalambiswa kadi nyekunduNemanja Vidic nje!!!
VIKOSI:
Chelsea: Cech, Ivanovic, Cahill, Terry, Azpilicueta, Ramires, Luiz, Willian (Matic 85'), Oscar (Mikel 67'), Hazard, Eto'o (Torres 78').
Subs not used: Cole, Lampard, Mata, Schwarzer.
Booked: Luiz
Goals: Eto'o 17', 45', 49'

Man Utd: De Gea, Rafael Da Silva, Evans, Vidic, Evra (Smalling 61'), Jones, Carrick, Valencia, Januzaj, Young (Hernandez 56'), Welbeck.
Subs not used: Giggs, Lindegaard, Cleverley, Fletcher, Kagawa.
Booked: Young, Valencia
Sent off: Vidic
Goal: Hernandez 78'

Referee: Phil Dowd

No comments:

Post a Comment