Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, October 28, 2013

ENGLISH PREMIER LEAGUE: SUNDERLAND 2 vs NEWCASTLE UNITED 1, HATIMAYE SUNDERLAND WASHINDA

Steven Fletcher kushoto akitupia kufunga goli la kichwa mapema dakika ya tano kipindi cha kwanza na kuitanguliza Sunderland kwa ushindi kipindi cha kwanza.Kocha mpya wa Sunderland Gus Poyet akishangilia bao hilo la Steven FletcherMathieu Debuchy scores the equaliser for Newcastle.
Dakika ya 57 kipindi cha pili Mchezaji wa Newcastle  Debuchy anaisawazishia bao Newcastle united baada ya mpira kupigwa na kuwapita mabeki wa Sunderland na hatimaye Debuchy kutokea nyuma na kufunga bao hilo. Dakika ya 84 Fabio Borini anaipachikia bao la pili Sunderland na kufanya 2-1 dhidi ya timu ya Newcastle United. Sunderland ambayo ilikuwa na kiu na ukame wa kushinda na ikiwa inashikilia nafasi ya mkiani inapata ushindi kwenye mtanange huu tena ikiwa ni mechi ya kwanza kushinda tangu  msimu huu uanze!!. Ushindi huu wa Sunderland unawaweka nafasi 19 wakiwa na pointi 4 na Newcastle nafasi  ile ile ya 10 wakiwa na pointi 11. Crystal Palace wanashikilia nafasi hiyo ya mkiani sasa.

No comments:

Post a Comment