Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, December 7, 2012

CHINA YATOA VIFAA VYA NGOMA ZA KITAMADUNI KWA TANZANIA.



Balozi wa China nchini Tanzania Lu Youiquing akimwangalia waziri wa habari utamaduni na michezo wa Tanzania Dr Fenella Mukangara jinsi ya avyopiga  gitaa, ambali ni moja ya  vifaa vya ngoma za utamaduni .
 
Balozi wa china nchini Tanzania Lu Youiquing amemkabidhi vifaa mbalimbali vya ngoma, muziki na filamu waziri wa habari, utamaduni na michezo katika Dr Fenella Mukangara kwa lengo la kuimarisha mahusiano katika nyanja za kitamaduni na filamu nchini.

Akiongea wakati wa mkutano wao na waandishi wa habari Balozi Lu Youiquing amesema vifaa hivyo mbali na kuendeleza sekta nzima ya burudani lakini pia vifaa hivyo vitasaidia kupunguza gharama za utayarishaji wa muziki na uhariri wa picha za filamu kwa wadau wa tasnia hizo.

Kwa upande wake Dr Mukangara amesema wamepokea vifaa vingi ikiwemo ngoma, magitaa na vifaa vingine ambavyo ni adimu nchini ambavyo vitaimarisha ubora wa filamu.

Amesema huo ni muendelezo wa mashirikiano na China katika mipango mbalimbali ya kukuza sekta ya ngoma, muziki na filamu.

Dr Fenera amesema baadhi ya vifaa vitapelekwa chuo cha sanaa na vingine vitapelekwa katika kitengo cha filamu kwa kuwa kuna baadhi ya vifaa ni kwa ajili ya kufanyia editing.

No comments:

Post a Comment