Makamu wa Rais Dkt. Nchimbi Aomboleza Kifo cha Jenista Mhagama; Atajwa Kuwa Kiongozi Aliyeheshimika
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, ameeleza kuwa Taifa
limepata pengo kubwa kufuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Peramiho
mkoani Ruvuma, marehemu Mhe. Jenista Joakim Mhagama (1967-2025).
Akitoa salamu za rambirambi nyumbani
kwa marehemu eneo la Itega, Jijini Dodoma, Makamu wa Rais alimwelezea Marehemu
Mhagama kama kiongozi aliyeheshimika na kutumikia nchi kwa uaminifu katika
majukumu mbalimbali ya kitaifa. Dkt. Nchimbi alisisitiza kuwa mbali
na kuwa Mbunge wa Peramiho, marehemu pia alitoa mchango mkubwa katika Chama Cha
Mapinduzi na kusimamia maendeleo ya Mkoa wa Ruvuma kwa ujumla.
"Marehemu Mhagama alikuwa
kiongozi aliyeheshimika na kutumikia nchi katika majukumu mbalimbali ya
kitaifa," alisema Makamu wa Rais, akisisitiza umuhimu wa kiongozi huyo
katika maisha ya kisiasa na maendeleo ya jamii.
Makamu wa Rais alitoa pole kwa
familia na waombolezaji, akiwaombea watoto wa marehemu na ndugu wa karibu Mungu
awape ujasiri wa kukubali jambo hilo, akitambua kuwa huo ni mwisho wa kila
mwanadamu.
Ratiba
ya Mazishi Kuendelea kwa Siku Nne
Kulingana na ratiba iliyotolewa na
Bunge la Tanzania, mwili wa Marehemu Mhagama ulitarajiwa kuwasili nyumbani
Dodoma (Itega) mnamo Desemba 12, 2025 saa 11:00 Jioni kwa ajili ya maombolezo.
Ratiba ya mazishi, ambayo inaendelea
hadi Desemba 16, 20257, inajumuisha hatua zifuatazo:
|
Tarehe |
Tukio Muhimu |
Mahali |
|
Desemba 13, 2025 (Jumamosi) |
Ibada, Salamu za Rambirambi na
Heshima za Mwisho |
Kanisa Katoliki, Kiwanja cha Ndege,
Dodoma. |
|
Safari ya kuelekea Songea Alasiri. |
||
|
Desemba 14, 2025 (Jumapili) |
Ibada na Maombolezo. |
Nyumbani kwa Marehemu Makambi,
Songea Mjini na Kanisa Katoliki Matogoro. |
|
Desemba 15, 2025 (Jumatatu) |
Ibada na Salamu za Rambirambi. |
Kanisa la Katoliki Peramiho,
Songea Vijijini. |
|
Wananchi wa Peramiho kuaga mwili. |
Kanisa la St. Joseph Peramiho,
Songea Vijijini. |
|
|
Desemba 16, 2025 (Jumanne) |
Mazishi. |
Kijiji cha Ruanda, Wilayani Mbinga. |
Makamu wa Rais Dkt. Emmanuel Nchimbi
anatarajiwa kuwa miongoni mwa viongozi wakuu watakaotoa salamu za rambirambi
wakati wa ibada za kumwaga marehemu Dodoma na Peramiho.



Post a Comment