Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, May 16, 2018

MAGUFULI KUKABIDHI SIMBA MWALI JUMAMOSI




RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli anatarajiwa kuikabidhi  Simba kombe la ubingwa wa Ligi Kuu Tanznaia Bara Jumapili Uwanja wa Taifa Dar es Salaam baada ya mchezo dhidi ya Kagera Sugar.
Hayo yalisemwa jana na Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Wallace Karia na kusema pia Dk. Magufuli atakabidhiwa kombe la ubingwa wa CECAFA na timu ya Vijana vya umri chini ya miaka 17, Serengeti boys.
“Tumemwandikia barua Rais kupitia kwa Waziri wa Habari, Sanaa Utamaiduni na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe kumwomba akubali kukabidhiwa kombe na timu ya Vijana U-17 Serengeti boys ililotwaa mwezi uliopita nchini Burundi,” alisema Karia
“Pia tumemwomba baada ya kukabidhiwa kombe hilo na Serengeti boys akubali kuikabidhi Simba lao baada kutwaa ubingwa wa ligi kuu msimu wa 2017-2018 kwani ndio mchezo wa mwisho katika ligi kucheza nyumbani,” aliongeza Karia.
Karia alisema wamemwomba Rais Dk. Magufuli apokee kombe hilo ili kuwapa morali wachezaji hao ambao wanajiandaa na fainali za Afrika mwakani ambapo Tanzania itakuwa mwenyeji.
Aidha alisema endapo Rais atakubali mchezo wa Ligi Kuu kati ya Simba na Kagera Sugar utaanza saa 8:00 mchana na kiingilio kitakuwa sh. 30000 mzunguko ili mashabiki wengi wapate fursa ya kuingia.
Hii itakuwa mara ya kwanza kwa Rais Dk Magufuli kuingia uwanja wa Taifa akiwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.

No comments:

Post a Comment