Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, April 24, 2018

ULINZI WAIMARISHWA KUELEKEA MECHI YA SIMBA NA YANGA


SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF)  limesema maandalizi ya mchezo wa watani wa jadi Simba na Yanga unaotarajiwa kuchezwa Aprili 29 yanaendelea vizuri.
Akizungumza leo Ofisa habari wa TFF, Cliford Ndimbo alisema mchezo huo unatarajiwa kuanza saa 10:00 jioni kwenye Uwanja wa Taifa lakini mageti yataanza kufunguliwa saa 2:00 asubuhi
“Jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es Salaam limesema ulinzi wa kutosha na kutoa tahadhari kwa wote wenye nia ya kufanya vitendo vya uovu,” alisema Ndimbo
Pia Ndimbo alisema mamlaka ya uwanja imethibitisha kuongezeka kwa camera ambapo sasa zimefikia 109 na zitakuwa zinafuatilia matukio yote ndani ya uwanja na kuwataka mashabiki wasiwe na hofu kwani kutakuwa na huduma ya vyakula na vinywaji ndani.
Aidha alisema tiketi zinaendelea kuuzwa kupitia Selcom na unatakiwa kujaza pesa kwenye kadi yako ya Selcom ambayo itakuweza kununua tiketi kupitia simu ya mkononi.
Viingilio katika mchezo huo ni Sh 30,000 kwa VIP A, VIP B na C ni Sh 20, 000 huku Mzunguko ikiwa ni Sh 7000 tu.

No comments:

Post a Comment