Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, April 24, 2018

OILERS YAONGOZA LIGI YA RBA


USHINDI wa michezo miwili katika wiki ya 11 ya Ligi ya mpira wa Kikapu mkoa wa Dar es Salaam (RBA) umetosha kuiweka kileleni Oilers kwa kufikisha pointi 26 katika michezo 13 iliyocheza.
Oilers iliifunga Kigamboni kwa vikapu 129-67 na Ukonga kwa vikapu 62-55 katika michezo iliyochezwa katika viwanja vya Bandari, Kurasini.
Savio inashika nafasi ya pili baada ya ushindi wa vikapu 58-44 dhidi ya ABC na kujikusanyia pointi 21 katika michezo 11 iliyocheza sawa na Vijana ambayo iliifunga Kurasini Heat kwa vikapu 90-56 ambayo imecheza michezo 12.
Pazi ambayo iliifunga UDSM insiders kwa vikapu 66-47 inashika nafasi ya nne baada ya kufikisha pointi 19 sawa na JKT ambayo iliifunga Mabibo kwa vikapu 62-51 na Magnet 96-69.
Ukonga kings inashika nafasi ya sita ikiwa na pointi 19 baada ya kuifunga Mabibo kwa vikapu 43-39, ABC na Mabibo baada ya kufungwa zimebaki na pointi 18 na Mannet licha ya kufungwa na Tanzania Prisons kwa vikapu 68-57 imebaki kwenye nafasi ya tisa  ikiwa na pointi 16.
Jogoo inashika nafasi ya 11 licha ya kufungwa na UDSM Insiders kwa vikapu 73-70 na Kigamboni licha ya kufungwa na Magone ambayo inaburuza mkia kwa vikapu 45-47.
Kwa upande wa wanawake JKT Stars baada ya kuifunga Ukonga Queens kwa vikapu 42-31 inaongoza ikiwa na pointi 11 baada ya kucheza michezo sita na kufungwa mmoja.
Ukonga Queens inashika nafasi ya pili ikiwa na pointi tisa, DonBosco Lionesses inashika nafasi ya tatu ikiwa na pointi saba, Vijana, Jeshi Stars na Oilers Princesses zina pointi tano.


No comments:

Post a Comment