Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, March 7, 2018

DRFA YAENDESHA KOZI YA GRASSROOT



MAKOCHA wa kozi ya grassroot wametakiwa kutumia vema elimu wanayopata kuendeleza vipaji vya soka Mkoa wa Dar es Salaam.
Hayo yalisemwa jana na Mwenyekiti wa Chama cha Soka Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) Almasi Kasongo alipokuwa akifungua kozi ya grassroot ya makocha wa soka inayoendeshwa na chama hicho.
“Mkoa wa Dar es Salaam tumepanga kuhakikisha tunaendeleza mpira kwa kuendesha kozi mbalimbali kwa makocha, waamuzi na uongozi hivyo kwa kuanza tumeanza na kozi ya grassroot hivyo ninyoi mliopata fursa hii mhakikishe mnakwenda kutumia elemu hiyo,” alisema Kasongo.
Pia Kasongo alisema baada ya kozi ya grassroot itafuatia kozi ya waamuzi ambayo itahusisha waamuzi vijana.
Kasongo alimshukuru mkufunzi Sunday Kayuni kwa kukubali kufundisha makocha hao 25 ambao watakuwa darasani kwa siku tano.
Kozi hiyo inafanyika kwenye Uwanja wa Karume, Dar es Salaam ilianza juzi na inatarajiwa kumalizika Jumamosi.



No comments:

Post a Comment