MOHAMED SALAH ASAINI LIVERPOOL
Salah, Raia wa Egypt mwenye Miaka 25, amesaini Mkataba wa Miaka Mitano na kutimiza azma ya muda mrefu ya Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp.
Dau la Uhamisho huu halikuvuka lile Dau la Rekodi ya Liverpool kumnunua Mchezaji kwa Bei Ghali ambalo waliliweka Mwaka 2011 walipomnunua Straika Andy Carroll kutoka Newcastle United.
Lakini Dau la Salah na Mchezaji mwingine wa Liverpool Sadio Mane anaetoka Senegal linalingana na kuwafanya ndio wawe Wachezaji wa Bei Ghali kutoka Afrika huko England.
Akiongelea Uhamisho huu, Jurgen Klopp ametamka: “Huu ni Uhamisho wa kufurahisha. Nimekuwa nikimfuatilia tangu aibuke huko Basle na amejengeka na kuwa Mchezaji Bora zaidi!”

Post a Comment