Haji Manara azungumza kuhusu ushindi wa Simba dhidi ya Yanga

Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Simba, Haji Manara jumatatu ya Februari, 27 amefanya mkutano na waandishi wa habari, ikiwa ni siku mbili tangu Simba na Yanga zilizokutana katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom, mchezo uliomalizika kwa Simba kuibuka na ushindi wa goli mbili kwa moja.
Katika mkutano huo Manara alizungumza mambo mbalimbali kuhusu mchezo huo lakini pia kuwataka mashabiki wa Simba kuendelea kuisapato timu yao ili waweze kutimiza malengo ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom kwa msimu wa 2016/2017.

No comments