Na Jumapili, ndani ya Old Trafford, Marcus Rashford, alipiga Bao 2 tena na kuweka Rekodi ya kuwa Kijana mdogo kabisa katika Historia ya Man United kufunga Bao za Ligi wakati Man United inawabonda Arsenal 3-2 Uwanjani Old Trafford.
NINI WAMESEMA BAADA YA KIPONDO HIKI:
Arsene Wenger kwa Arsenal:
"Tulitanguliwa kufungwa nah ii ilileta ugumu. Kinachosikitisha tulimiliki sana Mpira na kuruhusu Bao 3. Tumepoteza Pointi 3 muhimu hii Leo na inabidi tushinde Jumatano.”
Lejendari wa Arsenal Thierry Henry:
"Sidhani hili lingetokea enzi zote wakati nacheza. Huu si uchezaji wa Timu inayosaka Ubingwa. Hili ndio kama shabiki wa Arsenal nalitazama lakini sina hakika Timu hii inaweza kuwa Bingwa. Hakuonyesha! Lakini bado wamo mbio za Ubingwa lakini Leo walikuwa wa pili kwa kila kitu!”
Louis van Gaal:
"Nasikia fahari kubwa, nimeridhika na nina furaha kwa sababu tulifanya na Shrewsbury, tumefanya na Midtjylland na sasa tumefanya dhidi ya Timu nzuri sana ya Ligi Kuu England, nimefurahishwa!”
Marcus Rashford:
"Ilikuwa Gemu yangu ya kwanza kwenye Ligi na ni ajabu. Kupiga Bao 2 ni bonasi!"
No comments:
Post a Comment