Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, January 19, 2016

VPL MZUNGKO WA 15 KUENDELEA KESHO

Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, Maafande wa JKT Ruvu watawakaribisha Simba SC, Ndanda FC watakua wenyeji wa Mbeya City kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona.

Tanzania Prisons watakua wenyeji wa Coastal Union katika uwanja wa Sokoine jijini Mbeya, Stand United watacheza dhidi ya Toto Africans kwenye uwanja wa Kambarage, huku Mgambo Shooting wakiwakaribisha Azam FC kwenye uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.
Alhamisi ligi hiyo itaendelea kwa michezo mitatu, Mwadui FC watawakaribisha Kagera Sugar katika uwanja wa Mwadui, African Sports watakua wenyeji wa Mtibwa Sugar uwanja wa Mkwakwani jijini Tnaga, huku Young Africans wakiwakaribisha Majimaji FC katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment