Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, November 13, 2015

TSHABALALA MCHEZAJI BORA WA OKTOBA SIMBA

Beki wa kushoto wa Simba Mohamed Hussein 'Tshabalala'
Beki wa kushoto wa Simba Mohamed Hussein ‘Tshabalala’
Katika kuongeza morali na kuwazawadia wachezaji wanaofanya vizuri, klabu ya Simba ilianzisha tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwezi kuanzia mwezi wa Septemba 2015.
Mshindi wa mwezi wa Oktoba, 2015 ni Mohamed Hussen ‘Tshabalala’ ambapo alipigiwa kura nyingi na  mashabiki na wapenzi wa Simba na soka la Tanzania kwa ujumla kupitia simu za mkononi ambao pia wamejiunga na huduma ya Simba News.
Akizungumza leo jijini Dar es salaam Rais wa Simba Evans Aveva alisema “Uongozi, wanachama na wapenzi wa Simba wanathamini mchango wa wachezaji katika kuifanya timu yetu ifanye vizuri, hivyo tumeona ni jambo la busara kuwa klabu ya kwanza nchini Tanzania kuwa na tunzo za mchezaji wake bora.
“Tunaamini kuwa tuzo ya mchezaji bora wa mwezi wa Simba itaongeza ari na kujituma kwa wachezaji wetu. Sisi tukiwa kama viongozi ni kazi yetu ya msingi kuhakikisha kuwa wachezaji wetu hasa wale wanaojituma zaidi wanatambuliwa na kuenziwa’’.
Akizungumza jinsi tuzo ya mchezaji bora itakavyoendeshwa, Imani Kajula ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa EAG Group ambao ni washauri na watekelezaji wa Masoko na Biashara wa Simba, amesema: “Wanachama na wapenzi wa Simba na wapenda michezo ndio watakao kuwa wanachagua mchezaji bora wa mwezi kwa kutuma jina la mchezaji wanayempendekeza kwenda kwenye namba 15460”.
“Ni wale tu ambao wamejiunga na huduma ya Simba News kupitia mtandao wa Vodacom na Tigo wataweza kupiga kura kuchagua mchezaji bora wa mwezi wa Simba’’.
Simba News ni huduma iliyoanzishwa na Simba ili kuwapa wapenzi wa Simba habari mbalimbali za Simba popote pale walipo ikiwemo matokeo, majina ya wachezaji wanaocheza mechi, usajili na habari nyingine za klabu ya Simba.
Kujiunga na Simba News tuma neno Simba kwenda namba 15460 ni maalum kwa wateja wa Tigo na Vodacom pekee.

No comments:

Post a Comment