Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, May 9, 2015

SIMBA YAIFUNGA JKT RUVU NA KUVISHWA MEDALI




Wachezaji wa Simba wakishangilia bao lililofungwa na Awadh Juma kwenye mchezo dhidi ya JKT Ruvu uliochezwa Uwanja wa Taifa jana

Mshambuliaji wa Simba Emmanuel Okwi (kulia) akijaribu kumtoka beki wa JKT Ruvu, George Minja, katika mchezo wa kufunga pazia la Ligi Kuu ya Tanzania Bara mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam




Mwenyekiti wa Kamati ya Waamuzi wa Shirikisho la Soka Tanzania, Salum Umande Chama akimvalisha medali ya shaba mshambuliaji wa Simba Emmanuel Okwi pamoja na wachezaji wenzake baada ya kumaliza ligi wakishika nafasi ya tatu hafla iliyofanyika baada mchezo wa kufunga pazia la Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya JKT Ruvu uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Ligi, Fatma Abdallah.  (Picha zote na Rahel Pallangyo)
KLABU ya Simba imehitimisha safari yake kwenye Ligi Kuu ya Soka ya Tanzania Bara kwa ushindi baada ya kuifunga JKT Ruvu kwa mabao 2-1 kwenye mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam leo.
Hata hivyo matokeo hayo hayana maana yoyote kwa timu hizo kwani Simba imemaliza ligi ikiwa nafasi ya tatu na hivyo kukosa nafasi ya kuiwakilisha nchi kwenye mashindano ya kimataifa mwakani.
Wakati JKT Ruvu yenyewe pamoja na kufungwa imefanikiwa kubaki na pointi zake 31 na hivyo kuendelea kubaki kwenye ligi hiyo kwa msimu ujao.
Kwenye mechi hiyo isiyoshuhudiwa na mashabiki wengi JKT Ruvu ndio walitangulia kufunga kwa bao la Idd Mbaga aliyepokea krosi nzuri ya Ally Bilal kwenye dakika ya 15.
Lakini bao hilo lilidumu kwa dakika nne tu kwani Simba kupitia kwa kiungo wake Awadh Juma walifanikiwa kusawazisha bao hilo. Awadh Juma alisawazisha bao hilo baada ya kumalizia mpira uliotemwa na kipa wa JKT Ruvu Shaabani Dihile kufuatia shuti la Emmanuel Okwi.
Dakika tatu kabla ya mapumziko Simba walifunga bao la pili kupitia kiungo wa kimataifa wa Tanzania Said Ndemla aliyepata pasi nzuri ya Emmanuel Okwi.
Kwenye mechi hiyo timu zote zilifanya mabadiliko kadhaa kwa Simba kumtoa Twaha Ibrahim na kumuingiza Issa Abdallah na JKT Ruvu kumtoa Idd Mbaga na kumuingiza Cecik Ephraim.
Simba tena walimoa Wiliam Lucian na kumuingiza Mohamedi Hussein na JKT Ruvu waliwatoa Najim Maguli na Ally Bilal na kumuingiza Abdallah Makame lakini mabadiliko hayo hayakuweza kubadili sura ya mchezo huo.

No comments:

Post a Comment