Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, February 15, 2014

SIMBA YATOKA SARE NA MBEYA CITY, YANGA YAIFUNGA KOMOROZINE 5-2

Mchezo uliokuwa ukisubiriwa kwa hamu baina ya vilabu vya Simba na Mbeya City uliokuwa unachezwa hivi punde huko jijini Mbeya katika dimba la Sokoine umemalizika. Matokeo ya mchezo huo ni sare ya bao moja kwa moja, Mbeya City ndio walioanza kuliona lango la Simba katika dakika ya 13 kwa mkwaju wa penati likifungwa na Deogratius Julias , bao hilo lilidumu mpaka mapumziko wenyeji wakitoka kifua mbele.
simba-mpya-2
Kipindi cha pili Simba walianza kwa kasi na hatimaye katika dakika ya 50, mshambuliaji hatari wa Simba Mrundi Amiss Tambwe akaifungia timu yake bao la kusawazisha.
Timu hizo ziliendelea kushambuliana lakini mpaka refa anapuliza kipenga cha mwisho matokeo yalibaki moja kwa Mbeya City na moja kwa Simba.

KUTOKA COMORO
DSC_0051
Mabingwa wa Tanzania bara na wawakilishi wa nchi katika michuano ya kombe la mabingwa wa Afrika Dar Young African imefanikiwa kuvuka kwenda raundi ya pili ya michuano hiyo baada ya kuifunga timu ya Komorozine De Domoni mabao 5-2.

Mabao ya Yanga yamefungwa na Mrisho Ngassa aliyefunga hat trick, huku Hamis Kiiza na Msuva wakifunga bao moja moja.
Yanga sasa watakutana na timu kubwa ya Misri Naciona Al Ahly.

No comments:

Post a Comment