Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, February 17, 2014

CHAMA CHA NGUMI MKOA WA DAR ES SALAAM CHATAJA KIKOSI KITAKACHOSHIRIKI MAJIJI





MABONDIA 21 wakiwemo wanawake wanne wameteuliwa kuunda timu ya ngumi za ridhaa ya mkoa wa Dar es Salaam itakayoshiriki mashindano ya majiji yatakayofanyika Kampala, Uganda kuanzia Aprili 2 hadi 9 mwaka huu.

Mwenyekiti wa Chama cha ngumi Mkoa wa Dar es Salaam, Akaroly Godfrey alisema kuwa mabondia hao watafundishwa na makocha wanne watakaoongozwa na Frednand Nyagawa atakayesaidiwa na Anthony Kameda, David Yomba Yomba na Mazimbu Ally.
Mabondia hao ni Mussa Mchomanga (JKT), Omary Said (Green House) na Anthony Idoa (Magereza) watakaocheza uzito wa lightfly.

Katika uzito wa fly waliochaguliwa ni Hafidh Bamtula (Azimio), George Costantine (MMJKT) wakati katika uzito wa bantam waliochaguliwa ni Emilian Patrick (Mgulani JKT), Hamad Furahisha (Magereza) na Undule Lagson.

Uzito wa light waliochaguliwa ni Alex Michael (MMJKT) na Kassim Mbutike (MMJKT), katika uzito wa lightwelter ni Victor Njaidi , Haruna Hussein (Mgulani JKT) na Seleman Bamtula (Azimio). Katika uzito wa welter ni Mohamed Kibumbuli (Magereza) na Mussa Seif (Mavituuz).

Kwa upande wa uzito wa middle ni Hamidu Klahlfan (MMJKT) wakati uzito wa heavy ni Joseph Martin.
Kwa upande wa wanawake ni Grace Mwakamela, Sarah Andrew, Irine Mushin a Siwatu Kinde wote wa Makamo Makuu ya Jeshi la Kujenga Taifa (MMJKT)huku daktari wa timu hiyo ni Mussa Maila.

No comments:

Post a Comment