Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, February 17, 2014

MABONDIA JAPHET KASEBA NA THOMAS MASHALI WATAMBIANA



 
MABONDIA Japhet Kaseba na Thomas Mashali wametambiana kila mmoja kumpiga mwenzake mbele ya mashabiki waliofika kushuhudia pambano la kusheherekea siku nya wapendanao lililofanyika katika Ukumbi wa Mpo Afrika Temeke Dar es Salaam.

Mabondia hao walionesha dhahiri kutamani kupigana kwani walifika mahali kusema kama kuna promota anayetaka kuandaa pambano kati yao awaone ili wakubaliane.

“Mimi nakutamani kupigana na wewe hata sasa hivi kwani ulingo upo hapa ili nikufundishe ngumi zinavyopiganwa maana unatamba sana kwa vile unakutana na mabondia nyanya”, alisema Kaseba.

Kwa upande wa Mashali yeye alisema yupo tayari kupigana na Kaseba mahali popote kwani anajiamini atampiga kwa KO katika raundi za mwanzo tu.

Maneno ya mabondia hao yaliwavuta mashabiki waliofika ukumbini hapo kujionea mapambano yasiyokuwa na ubingwa ambayo yalikuwa maalum kusheherekea siku ya wapendanao na kutamani wangepanda ulingoni muda huo.

Japhet Kaseba ambaye aliwahi kuwa bingwa ngumi za mateke na baadae kuhamia kwenye ngumi za kulipwa  ameshacheza mapambano nane na kushinda matano huku matatu akishinda kwa KO na kupigwa kwa KO mapambano matatu.

Kwa upande wa Mashali ameshacheza mapambano 12 na kushinda mapambano tisa huku matano akishinda kwa KO, moja akatoka sare na kupigwa kwa KO mapambano mawili.

No comments:

Post a Comment