Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, February 17, 2014

LIGI DARAJA LA TATU MKOA WA TABORA YAFIKA PATAMU



LIGI daraja la tatu mkoa wa Tabora hatua ya nane bora inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Februari 23, mwaka huu katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Vita, Tabora.

Akizungumza kwa njia ya simu toka Tabora, Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Mkoa wa Tabora (TAREFA) Fate Remtullah alisema kuwa ligi hiyo itahusisha timu nane kutoka katika vituo vitatu.

“Ligi ya daraja la tatu hatua ya nane bora itaanza kuchezwa Februari 23, mwaka huu katika Uwanja wa Vita na hatutasikiliza sababu ya timu kushindwa kufika kwenye mchezo wake kwani tunataka tuwahi tarehe ya mwisho ya majina ya mabingwa TFF”, alisema Remtullah.

Msimu uliopita Tabora pamoja na baadhi ya mikoa iliathiriwa na mabadiliko ya mfumo wa uendeshaji wa ligi ikasababisha ligi kuchezwa kama bonanza ili kupata mwakilishi wa mkoa.

Timu zilizoingia kwenye hatua ya nane bora ni Reli Goweko FC, Mirambo FC, Magereza FC, Nzega FC, Abajalo FC, Manchester FC, Warumba FC na Chipukizi FC.

Pia alizishukuru timu zote zilizoshiriki ligi katika hatua ya makundi katika vituo vya Manispaa, Igunga na Sikonge pamoja na waamuzi kwa kufanikisha makundi kumalizika salama bila malalamiko.

No comments:

Post a Comment