Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, February 17, 2014

BLACK EAGLE YAIFUNGA ILALA FC, LIGI DARAJA LA TATU MANISPAA YA IRINGA



TIMU ya Black Eagle imeifunga Ilala FC bao 1-0 katika mchezo wa ligi daraja la nne Manispaa ya Iringa, mchezo uliochezwa Uwanja wa Samora.

Bao la Black Eagle katika mchezo huo lilifungwa na Hashim Chang’a katika dakika ya 10, bao ambalo lilidumu hadi dakika 90 ya mchezo.

Katika mchezo mwingine Isakalilo FC ilitoka sare ya kutofunga na Real FC katika mchezo uliochezwa uwanja wa Chuo Kikuu cha Elimu Mkwawa.

Akizungumza kwa simu toka Iringa, Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Manispaa ya Iringa, (IMFA) Rashid Shungu alisema kuwa ligi inaendelea vizuri kwani hawajapata malalamiko kuanzia ianze kuchezwa.

“Ligi yetu inaendelea vizuri na nashukuru hakuna malalamiko ambayo yamewasilishwa katika ofisi yangu hivyo naamini ligi itamalizika kama ratiba ilivyopangwa”, alisema Shungu.

Ligi hiyo inayofadhiliwa na aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Fredrick Mwakalebela inatajiwa kuendelea kesho kwa kuzikutanisha timu za Mtwa FC na Mtwivila City.

No comments:

Post a Comment