Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, November 11, 2013

JIJI LA MUNICH LAJITOA KUANDAA OLIMPIKI 2022

Mji wa Munich hautawania kuwa mwenyeji wa michezo ya Olimpiki ya majira ya baridi baada ya kushindwa kuungwa mkono na wakaazi wa mji huo katika kura ya maoni kuhusiana na iwapo mji huo uliingie katika kinyang'anyiro cha kuwania kuwa mwenyeji wa mashindano hayo.
 Meya wa jiji la Munich Christian Ude amesema kuwa juhudi za kuwa wenyeji wa michezo hiyo ya mwaka 2022, zimeshindwa baada ya wilaya zote pamoja na eneo la milima ya Alpine la Garmisch-Partenkirchen na Munich kupiga kura dhidi ya juhudi hizo baada ya mji wa Munich kuomba bila mafanikio kuwa mwenyeji wa mashindano ya mwaka 2018.
Ludwig Hartmann ni mwenyekiti wa wabunge wa chama cha kijani cha walinzi wa mazingira katika bunge la jimbo la Bayern na ambaye alikuwa akifanya kampeni dhidi ya uenyeji wa jiji la Munich katika michezo hiyo ya Olimpiki ya majira ya baridi. Hartmann amesema huu ni ushindi dhidi ya wanaotaka kufaidika na michezo hii.
"Kwa kweli hii si ishara dhidi ya michezo, ni ishara ya wazi kabisa dhidi ya hali ya kutokuwa na uwazi, dhidi ya watu wa kamati ya kimataifa ya Olimpiki IOC wanaotaka kufaidika na michezo hii, na leo ni siku ambayo viongozi wa kamati ya kimataifa ya Olipmiki wamepata pigo na sio pigo kwa michezo."
Munich ilijaribu kuwa mji wa kwanza kuwa mwenyeji wa mashindano ya majira ya joto na majira ya baridi ya Olimpiki, baada ya kuwa mwenyeji wa michezo ya Olimpiki ya majira ya joto mwaka 1972.
Wakati huo huo mwenge wa olimpiki kwa michezo ya mwaka 2014 ya majira ya baridi mjini Sochi umerejea duniani mapema leo.
 Chombo cha anga kilichowachukua wanaanga wa Urusi Fyodor Yurchikhin , mwanaanga wa Marekani Karen Nyberg na Mtaliani Luca Parmitano kilitua salama leo nchini Khazakhistan, hizi zikiwa ni taarifa kupitia shirika la mambo ya anga la Marekani NASA.
 Mwenge huo ulichukuliwa na wanaanga wawili katika mbio za kwanza za mwenge huo angani siku ya Jumamosi.
Na kwa taarifa hiyo ndio sina budi kusema tumefikia mwisho wa kuwaletea habari hizi za michezo jioni ya leo. Jina langu ni Sekione Kitojo , hadi mara nyingine kwaherini.

No comments:

Post a Comment