KLABU ya
Besiktas ya Uturuki imeshindwa rufani yao waliyokata kupinga kufungiwa na
Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA kwa kujihusisha na upangaji matokeo ya
baadhi ya mechi za ligi.Mahakama ya Usuluhishi ya
Michezo-CAS ilitangaza uamuzi wake wa kutupilia mbali rufani iliyokatwa na klabu
hiyo hivyo kuendelea na kifungo chao cha mwaka mmoja walichopewa na UEFA na
kufanya klabu hiyo kuenguliwa katika michuano ya Europa League msimu huu. Nafasi
yake katika hatua ya makundi itachukuliwa na klabu ya Tromso ya Norway pamoja na
kuwafunga katika mechi ya mtoano iliyochezwa jana. Klabu ya Fenerbahce nayo
nafasi yake itachukuliwa na klabu ya APOEL ya Cyprus baada ya wao pia kushindwa
katika rufani yao waliyopeleka CAS.
KUMBUKIZI YA DARAJA LA NYERERE 2016-2026
-
Daraja la Nyerere lililozinduliwa na aliye kuwa Rais wa Tanzania John
Pombe Magufuli Aprili 19, 2016. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)
Picha za Viongozi mba...
WASIRA AWATOLEA UVIVU WALIOANZA MBIO ZA URAIS
-
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Tanzania Bara, Stephen
Wasira, Leo Machi 27, 2026, Mjini Bunda Mkoa wa Mara alipokuwa akiweka
jiwe la ms...
Post a Comment