Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, July 17, 2013

WENGER ACHEMKA KWA FABREGAS


KLABU ya Arsenal inaonekana kama imechemka, katika mbio za kumwania nyota wake wa zamani, Cesc Fabregas, baada ya kutangaza kuwa haitashindana tena na Manchester United  katika mbio  za kumfukuzia nyota huyo.

Kutokana na hali hiyo, inaelezwa kuwa  inaweza kushuhudiwa, Fabregas akirejea  England akiwa katika jezi za Manchester United, baada ya kocha wa Gunners, Arsene Wenger kujiweka kando na kumuachia mpinzani wake, David Moyes amnyakue nyota huyo wa Barcelona akifahamu kuwa klabu yake itachukua nusu ya ada ya usajili wake.

Kwa mujibu wa gazeti la Daily Star, Manchester United imeshaweka mezani fungu la pauni milioni 26, kwa ajili ya kumnasa kiungo huyo ambaye alijiunga na klabu hiyo ya Nou Camp, miaka miwili iliyopita.

Arsenal ilisema jana kuwa kwa kurejesha fungu la pauni milioni 25 pamoja na asilimia  50, itakuwa ni faida kwao, baada ya kumuuza Fabregas kwa vinara hao wa Catalans kwa thamani ya pauni 30.

Wenger alisema jana kuwa hana tena mpango wa kumfuatilia tena Fabregas na hivyo kuiachia njia Manchester United.

Kwa mujibu wa vyanzo vya habari kwa upande wake, Barcelona nayo inaonekana kutoikubali kutoka klabu hiyo ya  Old Trafford, tangu ofa ya kwanza ya chaguo la kwanza la Moyes, Thiago Alcantara kukataliwa.
Pia kwa mazingira hayo, imebaki kushuhudiwa aidha kwa Fabregas, 26 akijiandaa kutua Manchester United akicheza kwenye nafasi ya kati  kama alivyokuwa  Arsenal.

Inaelezwa pia kwamba, Fabregas ni mchezaji ambaye amekuwa akiwindwa na kocha wa zamani wa Manchester United, Sir Alex Ferguson tangu timu hizo zilipokutana kwenye Uwanja wa  Old Trafford Oktoba  2004.


Kwa sasa Fabregas anasemekana kuwa miongoni mwa nyota kadhaa ambao wapo mguu nje mguu ndani katika klabu ya Barcelona, ambayo imetoa dau kubwa ili kumnasa nyota wa timu ya Taifa ya Brazil, Neymar huku ikiwa na  Lionel Messi.

No comments:

Post a Comment