Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, July 17, 2013

VIBOPA WANAOTESA NA TIMU KUBWA LIGI KUU YA UINGEREZA

Shahid Khan, mmiliki mpya wa timu ya  Fulham, akiteta na mmiliki mwenzake  wa timu ya  NFL,  Bob Kraft, kabla ya mtanange wa soka la  Marekani uliofanyika hivi karibuni mjini  Florida.
 BILIONEA, Shahid Khan usiku wa kuamkia juzi amekuwa tajiri mpya kuingia kwenye orodha ya mabilionea wanaomiliki timu za michuano ya  Ligi Kuu ya England. 

Arsenal — Stan Kroenke, Marekani KHAN OPENER ... new Fulham owner chats with fellow NFL boss Bob Kraft ahead of American football clash in Florida
Aston Villa — Randy Lerner, Marekani
Cardiff City — Vincent Tan, Malaysia
Chelsea — Roman Abramovich, Russia
Hull City — Assem Allam, Misri
Liverpool — John W Henry, Marekani  
Manchester City — Sheikh Mansour, Abu Dhabi
Manchester United — Malcolm Glazer, Marekani
Sunderland — Ellis Short, Marekani  
Hadi anaingia kwenye orodha hiyo, ilimlazimu Khan kujikamua kitita cha pauni milioni 150 ili kuchukua mikoba ya mmiliki wa zamani wa timu hiyo, Mohamed Fayed, ambaye ameamua kuiuza klabu hiyo ya Craven Cottage.

Mzaliwa huyo wa Pakistan, ambaye ni tajiri wa kuuza vipuri vya magari na mmoja kati ya vigogo wanaomiliki timu inayocheza Ligi  ya  NFL ya nchini Marekani, iitwayo  Jacksonville Jaguars, atakuwa ameungana na vigogo tisa wanaomiliki timu katika ligi hiyo.

Ifuatayo ni orodha ya vigogo wengine wanaomiliki timu hizo ambao Khan, (62), atapambana nao katika kutafuta mafanikio ya  soka nchini England, kama anavyofanya  nchini Marekani.



Katika klabu hiyo, Stan anamiliki asilimia 67  ya hisa za Arsenal, lakini tajiri huyo mkimya anazidiwa nguvu na bilionea raia wa Uzbek, Alisher Usmanov, ambaye huwa ndiye anayependa kuzungumzia kila kitu ndani ya klabu.

Kama alivyo Khan, Kroenke ana jina katika medani ya soka nchini Marekani, kwani naye pia anamiliki timu kwenye michuano ya ligi ya NFL, iitwayo St Louis Rams.

LERNING CURVE ... owner, far right, checks in on Villa training
Lerner (wa kwanza kulia) akiangalia mazoezi ya timu yake ya Aston  Villa.
Kabla ya kuinyakua timu hiyo, Lerner alikuwa miongoni mwa vigogo wanne waliokuwa wakiwania klabu hiyo ya Aston Villa tangu  Martin O’Neill aondolewe kwa maandamano mwaka  2010.

Mzaliwa huyo wa jiji la New York, ambaye ni mmiliki wa zamani wa timu ya Cleveland Browns, ilimlazimu kujikamua pauni milioni 300 ili aweze kukamata usukani wa kuiongoza timu hiyo.

.

VIN BONUS ... it's a red-letter day for Tan as Cardiff seal promotion
Tan aliibua hasira za mashabiki wa Cardiff, baada ya mwaka jana kubadilisha utamaduni wa kuvaa jezi za rangi ya bluu na kuvaa nyekundu  kwa lengo la kuendeleza imani ya ushirikina wa nchini kwao Malaysia.

Mbali na kubadili rangi  ya jezi, vilevile alibadili jina la kimichezo lililokuwa likitumiwa na klabu hiyo la  Bluebirds na kuwa Red Dragons.
Hata hivvyo imani yake hiyo ilimlipa mwaka jana, baada ya klabu hiyo ya ligi ya nchini Wales kuweza kuleta ushindani mkubwa katika mbio za kuwania ubingwa.



FAN-KS A MILLION ... supporters greet Rom following 2003 takeover
Mashabiki wa Chelsa wakimsalimia bilionea, Abramovich, baada ya kuinunua timu hiyo mwaka 2003.
Kwa ujumla Abramovich wakati alipoinunua timu hiyo kutoka mikononi mwa mfanyabiashara, Kenneth William Bates miaka kumi iliyopita, alionekana asingeweza kudumu nayo.

Hata hivyo, baadaye aliiwezesha Chelsea kutwaa mataji mbalimbali, yakiwamo ya Ligi Kuu, licha ya kukaliwa kooni na mashabiki kwa sera yake zake za kutimua makocha.

.

HULL OF A GUY ... Allam, left, is presented with chairman Russell Bartlett and son Ehab after buying City
Allam, (kushoto) akitambulishwa na Mwenyekiti wake, Russell Bartlett (katikati) na mwanaye, Ehab, baada ya kuinunua timu hiyo.
Allam alitua Hull City mwaka  2010, baada ya klabu hiyo kukumbwa na ukata kutokana na  kushuka daraja.
Hata hivyo, mmiliki huyo wa viwanda ambaye aliondoka nchini kwao Misri mwaka  1968, alilazimika kutumia pauni milioni 36 kwa ajili ya kuimarisha safu ya uongozi ndani ya klabu hiyo ya Tigers na mwaka jana fedha hiyo ilimlipa, baada ya kurejea tena Ligi Kuu.
.

TOP OF THE KOPS ... Henry, right, watches on with wife Linda Pizzuti
Henry (kulia) na mkewe,  Linda Pizzuti, wakishuhudia moja ya mechi za timu hiyo.

Kama ilivyo kwa matajiri wengine, Henry ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Fenway Sports Group na pia ni tajiri ambaye anamiliki timu katika ligi mbili.

Mmiliki huyo wa Liverpool, vilevile ndiye kiongozi mkuu wa timu ya Boston Red Sox na aliweza kuichukua klabu hiyo ya Anfield kutoka mikononi mwa raia wengine wa Marekani, Tom Hicks na George Gillett, mwaka 2010.
Hata hivyo, naye alijikuta akiingia utata na mashabiki wa timu hiyo, baada ya Mei mwaka jana kumtimua aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Kenny Dalglish.

Sheikh Mansour
Sheikh Mansour (wa pili kutoka kushoto mstari wa mbele) akiwasalimia mashabiki wa Manchester City siku ya kwanza alipowasili kwenye klabu hiyo ya Etihad.

Tajiri huyo kutoka familia ya kifalme nchi za Kiarabu, ameibadilisha mno klabu hiyo  ya Ligi Kuu tangu alipoichukua kutoka mikononi mwa Waziri Mkuu wa zamani wa Thailand, Thaksin Shinawatra.
Inaelezwa kwamba familia ya Mansour ina utajiri unaozidi wa Roman Abramovich mara sita na kwamba utajiri huo ndio ulioiwezesha timu hiyo kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu mwaka jana na pia umeifanya timu hiyo kuwa miongoni mwa timu zinazopigania ubingwa.
.

Malcolm Glazer
Mashabiki wa Manchester United wakiandamana dhidi ya utawala wa Glazer  mwaka  2010

Kibopa huyo raia wa Marekani aliichukua timu hiyo mwaka 2005 na ni mmoja wa wamiliki wenye mafanikio makubwa katika historia ya soka la England.

Hata hivyo, pamoja na kuandamwa na mashabiki, hasira hizo zilipungua mwaka jana alipoiwezesha timu hiyo kutwaa ubingwa wa 20 wa michuano ya Ligi Kuu ya nchi hiyo.


Ellis Short
Ellis akitabasamu mbele ya mashabiki baada ya kuinunua timu hiyo.
WARM WELCOME ... but Stan has not received blanket supportInaelezwa kuwa tajiri huyo ni kati ya matajiri ambao wanasaka mafanikio katika medani ya soka kwa udi na uvumba.
Hata hivyo umaarufu wa tajiri huyo raia wa Marekani unadaiwa kuongezeka zaidi baada ya kuinusuru Sunderland isishuke daraja mwaka huu.

No comments:

Post a Comment