Mechi ikitaka kuanza na hii ni lineup ya timu zote
REAL MADRID Jana walikuwa
huko England ambako walicheza Mechi ya Kirafiki na kuitwanga Bournemouth Bao 6-0
lakini mvuto mkubwa kwa Wanahabari ulikuwa ni kutaka kujua nini hatima ya
Straika wao kutoka Argentina Gonzalo Higuain.
Kwa Mwezi mzima sasa,
zipo ripoti kuwa Arsenal imefikia makubaliano binafsi na Higuain lakini hamna
chochote kati ya Klabu hizo mbili.
Na Jana, Meneja mpya wa Real Madrid Carlo Ancelotti amezipuuza ripoti hizo za kuuzwa Higuain na hasa kwa Napoli ambako Wiki hii ziliibuka Ripoti za Klabu hiyo ya Italy kutaka kuipindua Arsenal kwa kumnasa Higuain.
Huku akisisitiza kuwa yeye anataka Straika huyo abaki Real, Carlo Ancelotti alisema: “Si kweli. Kuhamia Napoli au Arsenal. Lazima tuongee kuwa Higuain ni Mchezaji wa Real hamna habari mpya. Ni Mchezaji muhimu kwetu.”
Katika Mechi yao ya Jana ambayo Real Madrid walishinda Bao 6-0 dhidi ya Timu ndogo Bournemouth, Bao za Real zilifungwa na Cristiano Ronaldo, Bao mbli, na Bao moja moja toka kwa Sami Khedira, Gonzalo Higuain, Angel di Maria na Mbrazil Casemiro.
Cristiano Ronaldo akifunga bao la kwanza
akipongezwa baada ya kufunga bao na wenzie jana
Mesut Ozil (kulia) nae akikatiza na hapa alionekana
kuwekewa na Simon Francis
Na Jana, Meneja mpya wa Real Madrid Carlo Ancelotti amezipuuza ripoti hizo za kuuzwa Higuain na hasa kwa Napoli ambako Wiki hii ziliibuka Ripoti za Klabu hiyo ya Italy kutaka kuipindua Arsenal kwa kumnasa Higuain.
Huku akisisitiza kuwa yeye anataka Straika huyo abaki Real, Carlo Ancelotti alisema: “Si kweli. Kuhamia Napoli au Arsenal. Lazima tuongee kuwa Higuain ni Mchezaji wa Real hamna habari mpya. Ni Mchezaji muhimu kwetu.”
Katika Mechi yao ya Jana ambayo Real Madrid walishinda Bao 6-0 dhidi ya Timu ndogo Bournemouth, Bao za Real zilifungwa na Cristiano Ronaldo, Bao mbli, na Bao moja moja toka kwa Sami Khedira, Gonzalo Higuain, Angel di Maria na Mbrazil Casemiro.
No comments:
Post a Comment