Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, July 17, 2013

MICHO AIMARISHA KIKOSI CHA KUIVAA TAIFA STARS, AITA TISA WAPYA, YUPO KAKA YAKE NA EMANUEL OKWI, WAANZA MAZOEZI LEO




Kocha Mkuu wa Uganda Cranes, Milutin Sedrojevic ameongeza wachezaji tisa katika kujiimarisha na mchezo wa marudiano dhidi ya Taifa Stars utakaochezwa Julai 27, mwaka huu utakaochezwa Uwanja wa Namboole mjini Kampala

Micho amesema kuwa mchezo huo wa marudiano na Tanzania  ni muhimu kwani umebaki kulinda heshima na kusafisha njia ya kufuzu klabu bingwa Afrika kwa wachezaji wa ndani.
"Ushindi wetu dhidi  ya Tanzania jijini Dar es salaam umenipa ujasiri kuelekea  hatua ya kufuzu, lakini kazi ni mbali na kumaliza", alisema kocha huyo mzaliwa wa Serbia.

Uganda the cranes waliifunga Taifa stars bao 1-0  lilifungwa na Dennis Iguma dakika ya 48 na timu hiyo imeanza mazoezi leo Jumatano asubuhi.

Micho amemwita  Augustine Nsumba, ambaye mara ya mwisho kuchezea  Cranes ni  mwaka 2006, kipa  kijana, Ismail Watenga, beki wa katikati, Hashim Ssempala na Willy Kavuma, na watatu toka kwa timu za U-23 ni winga wa kushoto,  Azizi Kémba na washambuliaji, Daudi Kasirye na Simon Okwi.
Wengine walioitwa kufanya mauaji dhidi ya Taifa stars ni Augustine Nsumba, Willy Kavumu, William Wadri and Habibu Kavuma

Uganda itawakosa Mshambuliaji, Patrick Mapafu, ambaye amekwenda nchini Ureno kufanya majaribio na Striker, Tonny Odur, ambaye alikuwa kikosi cha kwanza na Mapafu dhidi ya Tanzania ambaye alipata majeraha sasa nafasi yake itachukuliwa na ama Simon Okwi  au Daudi Kasirye.

Uganda itacheza mchezo wa kirafiki  Ijumaa kabla ya kuingia na kambini Jumatatu ijayo.
Timu Kamili iliyoitwa ni

Makipa ni : Muwonge Hamza (nyoka), Kimera Ali (SC VU) na Ismail Watenga (nyoka)
Mabeki: Wadada Nicholas (Sc nyoka), Iguma Denis (Sc Vu), Kasaaga Richard (Kiira Young Fc), Hashim Ssempala (Bul-Bidco), Yusuf Mukisa (Proline), Kawooya Fahad (KCC Fc), Kisalita Ayub (Villa) na Savio Kabugo (SC VU).

Mid fielders: Ntege Ivan (KCC), Majwega Brian (KCC FC), Kapteni Hassan Wasswa Mawanda (KCC FC), Mpande Joseph (nyoka), Muganga Ronald (Sc Villa), Kyeyune Said (URA), Azizi Kémba (Bul- Bidco), Augustine Nsumba (URA) na Willy Kavuma (Express).
Washambuliaji: William Wadri (Sc Vu), Simon Okwi (KCC), Daudi Kasirye (URA) na Frank Kalanda (URA).

No comments:

Post a Comment