Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, July 17, 2013

ARTETA: WENGER TUMIA PESA


 LONDON, England
MCHEZAJI, Mikel Arteta amempa somo kocha wa Arsenal,  Arsene Wenger akimueleza kuwa ni wakati muafaka kwa timu hiyo kujiunga kwenye msafara wa timu zinazotumia fedha nyingi.

Tayari kocha huyo wa  Arsenal, ameshatangaza kuachana na maisha ya ubahili aliokuwa nao kwa muda mrefu, akisema kuwa atafanya makubwa wakati wa usajili wa majira haya ya joto.
Kutokana na ahadi hiyo na Arteta hakusubiri kumpasha akisema kuwa ataupokea kwa mikono miwili usajili wa wachezaji nyota  kutokana na kwamba, anaamini kipindi hiki ni cha kupigania ubingwa.

Mhispania huyo kwa sasa anaonekana kubadili mawazo, baada ya miaka miwili ya hofu kuwa atakuwa nyota mwingine atakayeondoka.

 “Klabu imeshatangaza wazi kuwa tunataka kuwa tishio na mimi nalipongeza hilo.
“Baadhi ya wachezaji  tunaohusishwa nao wananifanya nijisikie mwenye furaha,” aliongeza.


Kwa sasa Gunners inadaiwa kujiandaa kutumia pauni milioni 35, kwa ajili ya kumnasa nyota wa  Liverpool, Luis Suarez  huku ikihusishwa kuwa kwenye harakati za kuwanasa, Gonzalo Higuain na Wayne Rooney. 

No comments:

Post a Comment