Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, July 17, 2013

CHEKI VIWANJA VINAVYOTARAJIWA KUCHEZEWA LIGI KUU MSIMU HUU VINAVYOONEKANA

Ally Hassan Mwinyi unavyoonekana kwa nje



VIWANJA sita vya soka vipo hatari kufungiwa na kamati ya ligi Kuu ya Tanzania Bara endapo wamiliki hawatavifanyia marekebisho.

Akizungumza jijini, akiwa ofisini kwake, Mkurugenzi wa Ligi hiyo Silas Mwakibinga alisema viwanja ambavyo vinaweza kufungiwa ni Ally Hassan Mwinyi -Tabora, Sheikh Abeid –Arusha, Kaitaba-Kagera, Sokoine – Mbeya, Jamhuri – Morogoro na Mkwakwani – Tanga.

“Hatutaona aibu kufungia viwanja ambavyo vitakuwa havikidhi kuchezewa Ligi Kuu kwa msimu wa 2013/14 hivyo wahusika wanatakiwa wahakikishe viwanja vinafanyiwa marekesho kama nilivyowajulisha kwenye barua”, alisema Mwakibinga

Pia alisema kiwanja  kina sababu inayofanya kufungiwa ikiwa ni pamoja na kukosa vyoo, maji, sehemu ya kuchezea kutokuwa nzuri na uzio wa kuzuia sehemu ya kuchezea na mashabiki.

Mwakibinga alitolea mfano uwanja wa Sheikh Abeid na Sokoine kuwa sehemu ya kuchezea nyasi zake ni mbaya kwani zinaota kwa kujenga matuta madogo madogo ambayo yanasababisha kupoteza uwelekeo wa mpira pindi unapodunda.

Uwanja wa Ally Hassan Mwinyi wa Tabora wenyewe hauna uzio wa kutenganisha sehemu ya kuchezea na sehemu wanazokaa mashabiki jambo ambalo kisheria halitakiwa hivyo unakosa sifa za kuchezewa Ligi Kuu.

Amewataka viongozi wa vyama vya soka kushirikiana na wamiliki wa viwanja hivyo ili kuvifanyia marekebisho kabla ukaguzi haujaanza kwani ukaguzi ukifika na kukuta bado havijarekebishwa watavifungia.
Kaitaba
 

No comments:

Post a Comment