Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, July 15, 2013

AFRIKA KUSINI NA ZIMBABWE ZATINGA NUSU FAINALI MICHUANO YA COSAFA

 Zimbabwe imefanikiwa kutinga katika hatua ya nusu fainali ya michuano ya Cosafa baada ya kufanikiwa kuwachapa Malawi kwa mikwaju ya penati baada ya kwenda sare ya bao 1-1 katika muda wa kawaida wa mchezo wao wa hatua ya robo fainali katika mchezo uliofanyika hii leo huko Kitwe nchini Zambia.

Ocean Mushure alifunga penato ya ushindi kwa washindi hao mara nne wa michuano hiyo.Katika muda wa kawaida  Zimbabwe walikuwa wa kwanza kushambulia na kuandika bao la uongozi kwa mpira wa kurudi uliofungwa na Masimba Mambare kunako dakika ya.Mshambuliaji wa Malawi James Sangala alitolewa nje yaw a uwanja baada ya kupewa kadi ya pili ya njano kabla ya mapumziko  kitendap ambacho kiliivuruga the Flames.

Lakini hata hivyo kunako dakika ya 85 ya mchezo , Boniface Kaulesi alifanikiwa kuandika bao la kuswazisha na mchezo kuelekea katika dakika za nyongeza na hatimaye kufikia katika hatua ya mikwaju ya penati. Katika hatua nyingine Afrika ya kusini nao wamefanikiwa kutinga katika hatua hiyo ya nusu fainali baada ya kuwachapa Namibia kwa bao 2-1 mchezo ambao pia umepigwa hii leo.Bafana Bafana walikuwa wakicheza mechi yao kwanza ya michuano hiyo kufuatia kupata nafasi ya kuingia moja kwa moja katika hayua hiyo

Mchezaji alieingia kutoka benchi Shongwe Jabulani aliandika bao kwanza kwa mpira mrefu muda mfupi baada ya kuanza kipindi cha pili.Afrika kusini pia wakafanikiwa kuandika bao la pili kupitia kwa Kekana Hlompho akiwa katika kona ya kisanduku cha hatari.

Namibia walifanikiwa kupata penati kufuatia Mkhwanazi Buhlke kuunawa mpira ndani ya kisanduku cha 18 lakini hata hivyoWilly Stephanus alishindwa kuandika bao kwa pigo la kwanza kabla ya mwamuzi kumtaka kurudia penati yake ambapo kiungo huyo aliiukwamisha mpira kambani.

No comments:

Post a Comment