Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, February 23, 2013

MUSA MUDDE NA FELIX SUNZU KUIONGOZA SIMBA KUIFUNGA MTIBWA SUGAR TAIFA LEO

 
 
Mshambuliaji wa Simba Felix Sunzu hii leo anatarajiwa kuwepo katika orodha ya wachezaji watakao itumikia timu hiyo katika mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar mchezo utakao pigwa uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Baada ya kuwa nje kwa kipindi kirefu akijiweka fiti.
Nafasi ya Sunzu kuwepo kikosini hii leo inakuja kufuatia mshambuliaji huyo raia wa Zambia kufanya vizuri katika mchezo wa kirafiki kati ya Simba na Mbeya City uliofanyika mkoani Mbeya.
Msemaji wa klabu ya Simba Ezekiel Kamwaga amesema kiwango kilicho onyeshwa na Sunzu katika mchezo huo ambao mwalimu Patrick Liewig aliwatumia wachezaji wengi wa kikosi cha pili Sunzu alionyesha kiwango ambacho kimempa matumaini makubwa mwalimu huyo ya kuanza kumuamini na kumpa nafasi ya kucheza.
Kiwango cha Sunzu katika siku za hivi karibuni mimeporomoka sana kutokana na kukabiliwa na maradhi ambayo yamemfanya kupigania afya yake kwa kipindi kirefu na sasa anaonekana kuwa ameaanza kuwa fiti.
Wakati hayo yakiwa hivyo, naye mlinzi tegemeo wa kati wa Simba Shomari Kapombe licha ya kuelezwa kuwa hali yake imeanza kuimarika kufuatia kupata matibabu ya kuondoa damu iliyovilia katika mishipa yake ya damu.
Hata hivyo mlinzi huyo wa hatakuwepo katika kikosi cha leo cha Simba kitakacho kuwa kikicheza dhidi ya Mtibwa Sugar kutokana na kwamba bado yuko katika uangalizi wa daktari wa Simba.
Hata hivyo Kamwaga amesema huenda mchezaji huyo akaanza kuingia dimbani katika mchezo wa marudiano dhidi ya FC Libolo ya Angola mchezo utakaochezwa Machi 2 jijini Luanda.
Mussa Mudde ambaye alikuwa kwao nchini Kenya amerejea jana na kujiunga na kambi ya klabu ya Simba.

Mudde alikwenda kwao kwa ajili ya kushiriki mazishi ya mwanae.
Hata hivyo nafasi ya Mudde kucheza mchezo wa leo dhidi ya Mtibwa haipo kufuatia uongozi wa Simba kumpa chaguo kama angependelea kufanya hivyo ama la kwa kuwa suala la kufiwa na mtoto lipewa uzito mkubwa na uongozi huo.

No comments:

Post a Comment