Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, August 19, 2023

Sky Force Tanga yawaangukia wadau wa michezo


Mkufunzi Ibrahim Kidiwa akizungumza na wachezaji wa Kituo cha Sky Force cha jijini Tanga hivi karibuni





Na Rahel Pallangyo

KITUO cha kukuza na kulea vipaji vya soka cha Sky Force cha jijini Tanga kimeomba wadau kuwasaidia vifaa vya michezo.

Kituo hicho chenye wachezaji 167 wenye umri wa kuanzia miaka 9-20 kinakabiliwa na uhaba wa vifaa vya kuchezea ikiwemo bips, koni, mipira na jezi wanafanyia mazoezi Uwanja wa Shule ya Sekondari Magaoni (Japan).

Mmoja wa wamiliki wa kituo hicho, Kombo Abdallah alisema yeye na wenzake Fakhi Amour na Ibrahim Kidiwa walianzisha kituo hicho kutokana na mapenzi makubwa waliyonayo katika mchezo wa soka.

“Tulianzisha kituo hiki kutokana na mapenzi yetu ya dhati kwa mchezo wa soka lakini kutokana na kipato chetu kuwa cha kawaida tunashindwa kumudu baadhi ya gharama za uendeshaji, hivyo tunaomba wadau watusaidie,” alisema Kombo.

Kombo alisema wachezaji wote wanafundishwa bure bila malipo yoyote na wamefanya hivyo kwa ajili ya kuwasaidia vijana kupata msingi mzuri wa soka.

Aidha, alisema pia wanafundisha vijana wanaopenda kuwa waamuzi wa soka na tayari wengine wameanza kuchezesha Ligi Daraja la Tatu Mkoa wa Tanga.

Timu ya kituo hicho kinashiriki ligi ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Mkoa wa Tanga na inashika nafasi ya saba kati ya timu 14 ikiwa na pointi nne huku vinara Fair Play ikiongoza kwa pointi tisa sawa na TFF Centre.

 

No comments:

Post a Comment