Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, January 11, 2013

NMB YADHAMINI BONANZA LA WACHEZAJI WA ZAMANI LITAKALOFANYIKA VIWANJA VYA SIGARA JUMAPILI





Benki ya NMB imekubali kudhamini bonanza la wachezaji wa timu zilizowahi kushiriki daraja la kwanza linalotarajiwa kuchezwa januari 13 mwaka huu kwenye viwanja vya Sigara, Temeke.

Akizungumza  jijini Mratibu wa bonanza hilo Kenedy Mwaisabula alisema tunatoa shukrani za dhati kwa banki ya NMB kwa kutambua mchango wa wachezaji wakongwe katika taifa hili na kukubali kuwapa sapoti.

"Tunaishukuru benki ya NMB kwa kutambua mchango wa wachezaji wa zamani kwa kukubali kudhamini bonanza hili", alisema Mwaisabula.

Timu za zamani ambazo zinashiriki kwenye bonanza hilo ni zile zilizowahi kutamba hapa nchini katika ligi kuu ya Tanzania ( zamani ligi daraja la kwanza) na litaanza saa 2:00 asubuhi, zinatakiwa kukamilisha ytaratibu zote ikiwa ni pamoja na kulipa ada ya ushiriki.

Timu hizo ni Simba, Yanga, Ushirika, Tukuyu stars, Pamba ya mwanza, Bandari ya Mtwara, Reli ya Morogoro, Pilsner, Coastal union, Kariakoo Lindi.

Pia alisema timu za simba, Yanga na Bandari ndio zimelipa ada za ushiriki hivyo kuomba zilizobaki kulipia mapema na amewataka mashabiki kufika kwa wingi kujionea burudani ya kandanda safi toka kwa wachezaji hao wa zamani.

Bonanza hili ni la pili kufanyika baada ya lile la kwanza lililofanyika Novemba 18 mwaka jana, ambapo Milambo ya Tabora ilifungwa magoli 3-2 na Bandari Mtwara, Reli Morogoro iliifunga Plisner ya Dar 1-0,Simba ilitoka sare na Kariakoo Lindi ya mabao 2-2 na Ushirika Moshi ilicheza na Kombaini baada ya kuwa na timu saba

No comments:

Post a Comment