Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, November 19, 2017

Wakenya Watamba Kilimanjaro International Airport Maratahon 2017

Na Mwandishi Wetu, Hai
WAKENYA wametamba katika mbio za kwanza za Kilimanjaro International Airport Marathon 2017 baada ya kushika nafasi za juu katika kilometa 21 na 42 kwa wanaume na wanawake.

Ushindi huo umefanya mamilioni ya fedha za zawadi kwenda nchini Kenya baada ya Duncan Kwemboi kushika nafasi ya kwanza katika mbio za kilometa 42 kwa kutumia saa 2:19:10 na Meshack Kirotich kumaliza wa pili kwa kutumia saa 2:21:25.

Mshindi wa tatu katika mbio hizo za marathon naye alikuwa Mkenya, Abraham Too aliyemaliza kwa kutumia saa 2:22:42.

Katika mbio za kilometa 42, ambazo mshindi wa kwanza hadi watatu aliondoka na Sh milioni 5, milioni 4 na milioni 3.

Kwa upande wa wanawake, katika kilometa 42 mbio hizo nazo zilitawaliwa na Wakenya,huku Failuna Abdi ndiye alikuwa Mtanzania aliyeshika nafasi ya juu baada ya kumaliza watatu katika mbio za kilometa 21.

Failuna alimaliza mbio hizo kwa kutumia saa 1:16:22 na kujinyakulia kiasi cha sh milioni 2, huku Dickson Marwa naye wa Tanzania alimaliza watano katika kilometa 21 kwa wanaume.

Marwa ambaye hivi karibuni alitamba katika mbio za Rock City Marathon na zile za Zanzibar, wakati katika mbio za KIA alipata sh milioni 1.5 baada ya kutumia saa 01:06:51.

Abdi akizungumza baada ya kumaliza mbio hizo alisema kuwa anasikitika sana kwa Wakenya kutawala mbio hizo kwani Watanzania kama wangejiandaa vizuri wangeweza kushinda.

Aliwataka wanariadha wa Tanzania kufanya mazoezi kwa bidii ili kuhakikisha wanafanya vizuri katika mbio zingine ndani na nje ya nchi.

Naye Marwa alisema kuwa ushindi ulikuwa mkali hasa kutoka kwa Wakenya ambao walikuwa wengi katika mbio hizo, lakini amefarijika kuwa Mtanzania aliyemaliza katika nafasi ya tano.

Katibu Mkuu wa Riadha Tanzania (RT), Wilhelm Gidabuday alisema kuwa mbio zimeanza vizuri kwa kushirikisha wanariadha wengi, lakini baadhi ya mambo hayakuandaliwa vizuri na kusababisha baadhi ya wanariadha waliomaliza mbio kutopewa medali zao kama walivyoahidiwa.

Mshindi wa mbio za kilometa 21 kwa wanaume, Mkenya Joel Kipmatai alisema kuwa mbio zilikuwa nzuri lakini hawakupata upinzani mkubwa kutoka kwa Watanzania.

Alisema mbio hizo zimeanza vizuri na zinatakiwa kurekebisha matatizo machache ili kuzidi kuziboresha na kuwa moja yam bio kubwa duniani miaka ijayo.

Mgeni rasmi katika mbio hizo za Kwanza za Kilimanjaro Internatinal Airport alikuwa Naibu Spika wa Bunge, Dk Tulia Nackson aliyekabidhi zawadi kwa washindi.

No comments:

Post a Comment