Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, September 16, 2017

SIMBA UWANJANI KESHO KUCHEZA NA MBAO FC




WEKUNDU wa Msimbazi Simba wanashuka dimbani kesho kuwakabili Mwadui FC katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Mchezo huo una umuhimu kwa kila timu kushinda pointi tatu ili kujiweka kwenye nafasi nzuri zaidi.
Simba imeonekana kuwa mbabe wa Mwadui hasa msimu uliopita baada ya kushinda michezo miwili, wa kwanza 2-1 kwenye uwanja wa Taifa na mwingine ulichezwa Kambarage Shinyanga na kushinda 3-0.
Timu hiyo ina pointi nne katika michezo miwili iliyocheza hivi karibuni ikishinda 7-0 dhidi ya Ruvu Shooting na kupata sare ya bila kufungana 0-0 dhidi ya Azam FC.
Mwadui ilishinda mchezo mmoja mabao 2-1 dhidi ya Singida United na kufungwa na Mtibwa Sugar 1-0 hivyo, ina pointi tatu.
Simba huenda ikamkosa mchezaji wake muhimu Haruna Niyonzima anayesumbuliwa na majeraha. Lakini ina furaha juu ya uwepo wa mshambuliaji wake hatari Emmanuel Okwi ambaye hakucheza mchezo uliopita kutokana na majukumu ya timu ya taifa.
Mbali na Okwi kuna Nicholaus Gyan ambaye anatabiriwa iwapo atacheza sambamba na Okwi basi wapinzani watapata wakati mgumu kuwadhibiti.
Simba inajivunia uwepo wa kipa wake mwenye kiwango kizuri Aishi Manula. Pia, mabeki iliyonayo Erasto Nyoni, Salim Mbonde, Method Mwanjali  huenda wapinzani wakapata wakati mgumu kupenya kirahisi.
Mchezo mwingine utakaochezwa leo ni Mbeya City dhidi ya Njombe Mji utakaochezwa kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
Njombe imetoka kupoteza michezo miwili kwenye uwanja wake wa nyumbani ikichapwa mabao 2-0 dhidi ya Prisons na 1-0 dhidi ya Yanga.
Mbeya City imeshinda mchezo mmoja dhidi ya Majimaji 1-0 na kufungwa mchezo mwingine dhidi ya Ndanda FC bao 1-0. Timu zote hizo kila moja inahitaji ushindi kujiweka kwenye nafasi nzuri.

No comments:

Post a Comment