Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, August 5, 2017

SINGANO ASAINI AZAM FC MIAKA MIWILI



 
MSHAMBULIAJI wa Azam FC, Ramadhan Singano ‘Messi’ ameongeza mkataba wa miaka miwili kuendelea kuitumikia klabu hiyo baada ya kukwama kusaini mkataba na El Jadidi ya Moroco alikofauli majaribio yake.
Singano alirejea jijini Dar es Salaam juzi baada ya wakala wake kutokuwa mwadilifu katika makubaliano ya kimkataba kwani inadaiwa aliongeza dau mara mbili ya ile waliyokubaliana awali.
Akizungumza na gazeti hili, Ofisa habari wa timu hiyo Jaffa Idd alisema uongozi umeamua kumpa mkataba mpya kwa sababu wakati anaondoka aliaga na akapata baraka zote na akaambiwa endapo atakwama anaruhusiwa kurudi.
 “Singano tulimwambia akikwama arudi nyumbani tutampa mkataba, kijana wetu alikwenda kutafuta maisha lakini mambo yamekuwa tofauti na matarajio yake, alichanganyikiwa ila anapaswa kutulia acheze mpira,” alisema Jaffar Idd
Naye Singano amekiri kuongeza mkataba na kuishukuru Amaz kwa kuonesha utu kwa hata alipokuwa Morocco walikuwa wanamfuatilia kwa karibu.
“Ni kweli nimepewa mkataba mpya, Azam wamenifanyia utu kwani hata nilipokuwa Morocco walikuwa wakiwasiliana na mimi kujua maendeleo yangu, hata nilipokuwa naondoka waliniahidi hilo kwamba nikishindwa nirudi nyumbani,” alisema Messi
Singano atakuwemo kwenye kikosi cha Azam ambacho kitaondoka kesho kwenda Kampala, Uganda kuweka kambi maalumu ya maandalizi ya msimu mpya wa ligi utakaonza Agosti 26.

No comments:

Post a Comment