Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, August 8, 2017

SHIJA RICHARD AWEKA SERA ZAKE BAYANA ENDAPO ATACHAGULIWA KUWA RAIS TFF




MGOMBEA wa Urais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Shija Richard Shija amesema atajenga shule ya kukuza vipaji na kuviendeleza mkoani Dodoma na kila mkoa ataajiriwa mratibu wa soka.
Shija aliyasema hayo jana wakati akizindua kampeni zake na kusema ili upate matokeo mazuri katika soka lazima wachezaji waanze kuandaliwa wakiwa na miaka sita hivyo ataweka mfumo rasmi wa kukuza na kuendeleza vipaji.
“ Kampeni zangu zitajikita katika kutangaza mambo ya kisera ya TFF badala ya masuala ya kiutendaji kwani mafanikio  katika soka sio jambo la kufumba na kufumbua,” alisema Shija.
Shija alisema Tanzania ina changamoto kubwa katika mfumo rasmi wa kutambua na kuendeleza wachezaji hivyo amekuja na mpango wa muda mrefu na muda mfupi.
Pia Shija alisema mratibu wa soka atakayeajiriwa kila mkoa atakuwa anaripoti kwa mkurugenzi wa ufundi wa TFF  na atakuwa na jukumu la kutoa mapendekezo ya wachezaji wanaostahili kupelekwa katika shule ya vipaji.
Aidha Shija alisema atasimamia na kutekeleza Azimio la Bagamoyo lililoanzishwa na uongozi uliopita kwa sababu linagusa mambo muhimu ya kuendeleza soka.
Alisema ataimarisha misingi imara mikoani kwa sababu mikoani ndiko unakochezwa soka kwa hatua za awali ili kuongeza ari ya kushiriki na kuwekeza katika michezo.
Alisema atajenga miundombinu na mazingira rafiki ya kucheza mpira na kuwashawishi wazazi kuwekeza na kuwaruhusu watoto wao wenye vipaji waingie kwenye michezo.
Shija alisema atahakikisha timu zinaajiri watendaji wenye weledi wa kutosha na kuahidi kushirikiana na vyama wanachama wa TFF na kuimarisha soka.


No comments:

Post a Comment