Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, August 7, 2017

NIYONZIMA ASEMA TUKUTANE UWANJANI




KIUNGO mpya wa Simba, Haruna Niyonzima amesema hawezi kuongea chochote ila majibu ya maswali yanayoulizwa juu yake atayaosha uwanjani kuanzia leo.
Niyonzima aliyasema hayo jana alipozungumza Wandishi wa Habari katika makao makuu ya klabu hiyo alipokuwa akitambulishwa pamoja na nyota wengine Emmanuel Okwi na Nicholas Gyan.
Kiungo huyo ambaye ametokea Yanga baada ya kumaliza mkataba wake alisema kwa sasa yeye ni mali halali ya Simba na mambo mengine atajibu uwanjani.
“Mimi ni mchezaji halali wa Simba, sina mengi zaidi ya kuongea kikubwa tukutane uwanjani,” alisema Niyonzima.
Niyonzima, Okwi na Gyan wanatarajiwa kuongeza hamasa ya mashabiki wa katika mchezo wa kirafiki utakaochezwa leo dhidi ya Rayon Sports ya Rwanda katika Tamasha la Simba Day.
Kila Agosti 8, klabu ya Simba hufanya tamasha hilo ambalo hutumika kutambulisha kikosi chao pamoja na kutambulisha jezi.
Niyonzima alikuja jana na kuanza mazoezi leo asubuhi na kikosi hicho katika Uwanja wa Boko Veterani, Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment