Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, August 7, 2017

MULAMU ASEMA ATAENDELEZA SOKA LA VIJANA NA WANAWAKE




MGOMBEA nafasi ya Umakamu wa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Mulamu Nghambi ameahidi kuinua soka la vijana, wanawake pamoja na kuendeleza miradi ya michezo nchini.
Nghambi alisema hayo leo wakati akizindua kampeni zake katika Ukumbi wa habari maelezo Wandishi wa Habari kuhusiana na kile anachotarajiwa kukifanya pindi akichaguliwa.
Alisema, kwa muda mrefu maendeleo ya soka la vijana na wanawake kwa ujumla yamekuwa yakisuasua na yanahitaji mwamko ambao akichaguliwa atahakikisha unakuwapo.
Alisema, ana uzoefu wa muda mrefu katika kuendeleza soka ambapo mwaka 1999 hadi 2000 alikuwa meneja msaidizi wa klabu ya Simba na kusha kuja kuwa msaidizi wa masuala ya kifedha.
Alisema, amewahi kuwa mjumbe wa kamati ya vijana wa TFF, mjumbe wa kamati ya kusaidia timu ya taifa ishinde,Mwenyekiti wa chama cha Soka cha Dodoma, Mjumbe wa kamati ya mabadiliko ya Simba.
Kuhusiana na kanuni iliyowekwa na Baraza la Michezo la Taifa(BMT) inayozuia mtu kuwa na kofia mbili katika mchezo wa soka, Nghambi alisema kuwa ataachia nafasi ya uenyekiti akishinda nafasi yake hiyo ya Umakamu wa Rais.
Pia aligusia uhusiano wake na klabu ya Simba hasa katika kuangalia ni kwa kiasi gani hautoweza kuwa na mgongano wa kimaslahi iwapo akichaguliwa kushika wadhifa huo wa Umakamu, alisema kuwa yeye ni mwadilifu na hatochanganya mambo hayo mawili.
Alisema, atafanya kazi na kila mtu, kila timu, kila kundi, kila klabu na kila chama ili mradi wawe na malengo ya kuendeleza soka la hapa nchini.
Alisema atahakikisha kuwa anaimarisha mifumo bora zaidi ya uchumi wa klabu na vyama vya michezo ikiwa pamoja na kuinua ligi daraja la kwanza, la pili hasa katika kuwatafutia wadhamini.
Alikosoa mfumo wa sasa wa uendeshwaji wa soka kwa kuwa umegubikwa na uzamani hasa kutokana na kuwa kila Mkoa una dira yake inayofuata katika  kuendesha soka.
Alisema, atahakikisha kuwa anajenga dira moja ya kitaifa itakayoziwezesha klabu za Soka kuwaendeleza wachezaji na wanafunzi wa soka kupata soko la uhakika ndani na nje ya nchini.

No comments:

Post a Comment