Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, May 21, 2017

MOURINHO: ROONEY ANA WAKATI MGUMU SANA

Image result for wayne rooney
KOCHA wa Manchester United, Jose Mourinho amesema kwamba nahodha wa klabu hiyo, Wayne Rooney, ana wakati mgumu sana kisoka.
Mourinho ambaye amekuwa akimbania Rooney kwa kumwacha nje kabisa ya kikosi au kumweka benchi, amesema kwamba mchezaji huyo anaelekea kwenye siku za mwisho za kucheza soka ya ushindani, hivyo anatakiwa kuwa makini kisaikolojia.
Rooney anaweza kuondoka United kiangazi hiki ikiwa hataridhika na idadi ya mechi au dakika anazopangiwa kucheza, na Everton alikozaliwa wanamtaka, lakini pia Ligi Kuu ya China inaweza kumpata na kumpatia kiasi kikubwa cha fedha.
Imedaiwa pia kwamba Mourinho alikuwa akipanga kumkosesha ‘send off’ leo watakapomaliza Ligi Kuu ya England (EPL) kwa kucheza na Crystal Palace, kwani anadaiwa kutaka kumwaga uwanjani makinda.
Mourinho alipoulizwa iwapo Rooney angecheza leo alisema: “Sijui. Alicheza dakika 90 kwenye mechi iliyopita (dhidi ya Southampton) kwa hiyo labda hapana. Nitachukua wachezaji watatu au wanne wa kikosi cha kwanza na kila mmoja atacheza nusu ya mechi ili kukipa kikosi uzoefu kidogo, lakini nataka kuwaacha wachezaji kwa ajili ya Jumatano (fainali ya Ligi ya Europa dhidi ya Ajax).
Mourinho amejumuisha chipukizi 10 kwenye kikosi cha wachezaji 18 wa kuivaa Palace, nao ni Axel Tuanzebe, Tim Fosu-Mensah, Joel Pereira, Kieran O’Hara, Demetri Mitchell, Scott McTominay, Josh Harrop, Matty Willock, Angel Gomes na Zak Dearnley.
Kadhalika amesema kwamba Zlatan Ibrahimovic, pamoja na majeruhi wengine, Marcos Rojo, Luke Shaw na Ashley Young, watasafiri na timu kwenda Stockholm kwa ajili ya mechi hiyo ya Jumatano.

No comments:

Post a Comment