Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, March 11, 2017

YANGA MHHH, SIJUI!!!






SAFARI ya Yanga kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika imepata hitilafu baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Zanaco ya Zambia katika mechi ya raundi ya kwanza iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Matokeo hayo yanailazimisha Yanga kupata ushindi wowote katika mechi ya marudiano itakayochezwa mjini Lusaka mwishoni mwa wiki ijayo ili kusonga mbele.
Simon Msuva alikuwa wa kwanza kuiandikia Yanga bao la kuongoza katika dakika ya 38 akiunganisha pasi ya Justin Zullu kabla ya kuujaza mpira wavuni.
Zanaco ilipata bao lake la kusawazisha katika dakika ya 78 likifungwa na Atram Kwame baada ya kuunganisha vema pasi ya Ernest Mbwewe na kuujaza mpira wavuni.
Katika mechi hiyo wageni walitawala katika vipindi vyote na walionekana kukamilika kila idara hali iliyoisumbua Yanga na kuonyesha kwamba wanatakiwa kujiandaa na kuwa makini katika mechi ya marudiano kwani wachezaji wake walionekana kuwahi kuchoka.
Yanga ilianza kulishambulia lako la Zanaco dakika ya 11 kupitia kwa kiungo wake Thaban Kamusoko ambaye hata hivyo nafasi nzuri aliyopata alishindwa kuitumia. Dakika moja baadae Zanaco pia ilikosa bao kupitia kwa mchezaji wake Saith Sakala lakini shuti lake lilipanguliwa kiustadi na kipa wa Yanga Deogratius Munishi ‘Dida’.
Augustino Mulenga nusura aifungie Zanaco bao katika dakika ya 18 lakini akiwa kwenye nafasi nzuri alipiga shuti dhaifu lililoishia mikononi mwa Dida.
Yanga: Deogratius Munishi ‘Dida’, Hassan Kessy, Mwinyi Haji, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Vincent Bossou, Kevin Yondan, Simon Msuva, Justin Zulu, Donald Ngoma/Emmanuel Martin dk58, Thabani Kamusoko/Juma Mahadhi dk60 na Obrey Chirwa.
Zanaco: Racha Kola, Ziyo Kola, Zimiseleni Moyo, Chongo Chirwa, Saith Sakala/Kennedy Musonda dk69, Taonga Mbwemya, Richard Kasonde, Attram Kwame, Augustine Mulenga, Ernest Mbewe na George Chilufya. 

No comments:

Post a Comment