Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, November 8, 2016

TASWA YAMLILIA MZEE SAID MOHAMED WA AZAM FC

 Image result for MOHAMED AZAM FC IMAGES
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
CHAMA Cha waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), kimepokea kwa masikitikio makubwa taarifa za kifo cha Mwenyekiti wa klabu ya Azam FC na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Kuu, Said Muhammed Abeid,  kilichotokea  jana Novemba 7, 2016 alasiri katika Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam.
Atakumbukwa na waandishi wa habari za michezo kutokana na ukaribu wake na wanahabari na alikuwa na ushirikiano wa kutosha pale alipoombwa kufanya hivyo,  alikuwa kiungo kikubwa kwa TASWA kufanikisha matukio mbalimbali ya udhamini.
TASWA inatoa pole kwa familia ya marehemu, klabu ya Azam na wanamichezo wote hapa nchini katika kuomboleza kifo cha Mzee Said, huku tukiwatakia moyo wa subira katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.
 
Itoshe kusema tumepoteza mtu muhimu sana, ambaye  mchango wake na uhodari havitasahaulika kwa wadau wa michezo.

No comments:

Post a Comment