Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, August 22, 2016

YANGA UWANJA KUKAMILISHA RATIBA KESHO





YANGA kesho inashuka dimbani kumaliza ungwe ya mwisho hatua ya makundi Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kwa ajili ya kusaka heshima.
Mchezo huo utachezwa saa tisa na nusu jioni kwa saa za Afrika Mashariki kwenye uwanja wa Stade TP Mazembe.
Ni mchezo wa kusaka heshima kwa kuwa wamekwishatolewa kwenye mashindano, timu mbili zilizofuzu  ni TP Mazembe yenye pointi 10 na Medeama ya Ghana yenye pointi nane ambazo ikiwa Yanga itashinda au kupoteza haiendi popote na wala hatazifikia.
Katika mchezo wa kwanza Yanga ilipoteza dhidi ya timu TP Mazembe kwenye uwanja wa Taifa, baada ya kufungwa bao 1-0. Ni mchezo ambao Yanga itamaliza kwa heshima kama itashinda ikiwa na pointi saba.
Ikumbukwe mwaka 1998 Yanga ilishiriki Ligi ya Mabingwa Afrika na kufikia hatua hiyo lakini  haikushinda mchezo hata mmoja.
Mwaka huu inaonekana kuna mabadiliko baada ya kushinda angalau mchezo mmoja dhidi ya TP Mazembe na kupoteza miwili dhidi ya Medeama na Mazembe na kupata sare moja dhidi ya Medeama kwenye uwanja wa nyumbani, Taifa.
Timu zilizoko kwenye kundi moja A, Medeama itachuana na Mo Bejaia nchini Algeria kumaliza mchezo wa mwisho, lakini kama Medeama itashinda au kutoka sare itajiongezea pointi lakini kama Mo Bejaia yenye pointi tano itashinda basi zitalingana kwa pointi hivyo, mshindi huenda akaamuliwa kwa idadi ya magoli.
Kocha wa Yanga Hans Pluijm alisema licha ya kutolewa hakuwezi kuwakatisha tamaa na kushindwa kufanya vizuri katika mchezo wa mwisho.
Alisema ushindi ni muhimu sio tu kwa timu kuweka rekodi bali hata kwa wachezaji watakaocheza kwa juhudi ni nafasi yao kujiuza. 
“Tunahitaji kushinda mchezo huu na tunauchukulia kwa ukubwa ili tumalize salama na kujiwekea rekodi ya kipekee,”alisema.

No comments:

Post a Comment