Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, August 27, 2016

SIMBA YATOKA SARE NA JKT RUVU TAIFA




MATOKEO ya sare ya bila kufungana yameifanya Simba ya msimu huu isiwe na tofauti na ile ya msimu uliopita ambapo ilikuwa ikipata matokeo yake kama homa ya vipindi.

Simba ilianza ligi kwa ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Ndanda katika mechi ya kwanza lakini jana ilishindwa kuendeleza wimbi hilo la ushindi baada ya kulazimishwa sare ya bila kufungana na JKT Ruvu katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Huku mashabiki wake wakitarajia kupata ushindi jana, walijikuta wakitoka uwanjani mapema na wengine kutoka vichwa chini baada ya matokeo hayo.

Katika mechi ya leo Simba ilitawala karibu katika kila idara kuanzia dakika ya kwanza ya mchezo lakini wachezaji wake walikosa mabao mara kadhaa kila walipolifikia lango la wapinzani wao.

Ni katika kipindi cha kwanza mchezaji Shizza Kichuya alipoteza nafasi kadhaa za kufunga hasa ile ya dakika ya 36 ambayo aliwalamba chenga mabeki wa Ruvu lakini alishindwa kumalizia na kuporwa mpira huo.

Mbali na Kichuya, Laudit Mavugo naye alipoteza nafasi nyingi za kufunga mbele ya JKT Ruvu ambayo wachezaji wake walicheza kwa kujihami muda wote huku washambuliaji wake Atupele Green na Saad Kipanga wakishindwa kupiga shuti hata moja langoni mwa Simba.

Kutoka kwenye uwanja wa CCM Kirumba Mwanza, Mwadui iliibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mbao FC. Bao la Mwadui liliwekwa kimiani na Abdallah Seseme katika dakika ya 29 Kwenye uwanja wa CCM Kirumba Mwanza.

Ligi hiyo inaendelea tena leo ambapo bingwa mtetezi Yanga itashuka kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam kucheza na African Lyon.

Yanga inapewa nafasi ya kuibuka na ushindi katika mechi ya leo kutokana na ukweli kwamba bado iko vizuri kwa vile imetoka kushindana michuano ya kimataifa.

Timu hiyo ilitupwa nje kwenye Kombe la Shirikisho na TP Mazembe ya Congo DR baada ya kufungwa mabao 3-1 lakini hilo haliondoi ukweli kwamba timu hiyo bado ipo vizuri na ina uwezo wa kutetea taji lake.

No comments:

Post a Comment