Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, August 16, 2016

MANZANDA AIGARAGARAZA KAMATI YA UCHAGUZI YA TFF



KAMATI  ya Rufani za uchaguzi Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imetengua maamuzi ya kamati ya uchaguzi ya TFF kuhusu uchaguzi wa Chama cha Soka cha Kinondoni, KIFA na kudai kamati hiyo imekiuka katiba ya TFF.
Akizungumza wandishi wa habari, Mwenyekiti wa kamati ya rufani za uchaguzi,   Wakili Julius Lugaziya alisema kamati ya uchaguzi ya TFF kikanuni haina mamlaka ya kutengua, kusitisha uchaguzi wa vyama vya wilaya kwani siyo mwanachama wa TFF.
"Kamati ya rufani ilipokea rufani toka kwa Thomas Manzanda ikasikiliza pande mbili ambayo ni TFF iliwakilishwa na wakili Edward Muga na Manzanda ikagundua kuwa rufani imekuja nje ya muda lakini kutokana na mamlaka iliyonayo ikaona kuna jambo la muhimu hivyo ikaendela kuisikiliza", alisema Lugaziya.
Wakili Ligaziya alisema kamati imetengua maamuzi ya kamati ya uchaguzi ya TFF hadi rufaa ya Thomas Manzanda itakaposikilizwa na kamati ya rufani ya DRFA ambayo imepewa siku 14 tangu kamati hiyo ilipotoa maamuzi Agosti 15.
Kabla ya kusoma maamuzi hayo Mwenyekiti  Lugaziya alisema mwendeno wa rufaa hiyo ulivyokuwa na kusema Wakili wa TFF, Edward Muga alijaribu kuishawishi kamati yake kuwa maamuzi ya kamati ya uchaguzi yalikuwa sahihi lakini Lugaziya akasema kamati hiyo imekiuka kanuni za TFF ibara 52 kifungu cha sita.
Wakili Lugaziya alisema kamati ya uchaguzi ina mamlaka ya kuingilia uchaguzi wa wanachama wa TFF endapo kuna malalamiko katika mchakato wa kuwapata wagombea, rushwa, haki ya kutosikilizwa kwa wagombea (natural justices) na endapo matokeo yatakuwa ya kughushi.
Wakili Lugaziya alifika mbali na kudai Kamati ya uchaguzi na TFF haikupata malalamiko bali ilipata nakala ambayo ilitumwa kwa kamati ya rufaa hivyo ilikaa kama kamati ya rufani mamlaka ambayo haikuwa nayo .
Uchaguzi wa Chama cha Soka cha Kinondoni ulifanyika kwa mara ya kwanza Juni 12 lakini kamati ya uchaguzi ya KIFA ikatengua matokeo yake baada ya kugundua kura zimezidi idadi ya wapiga kura, ukarudiwa tena Julai 18 ambapo Kamati ya Uchaguzi ya TFF ilitengua na kuagiza uchaguzi urudie na nidhamu zichukuliwe kwa watu mbalimbali  kinyume na kanuni za TFF.
Baadae ya kutengua matokeo ya Julai 18, Kamati ya Uchaguzi ya TFF iliitisha kikao cha maridhiano kwa kutumia barua ambayo haikuwa yake na idadi ya watu waliotakiwa kufika bila kusema mkutano utafanyika wapi wala muda wa mkutano na bila kuwashirikisha walioandika barua
Pia Kamati  ilipitisha uamuzi wa kufanyika uchaguzi upya huku ikijua kuwa Manzanda amekata rufaa DRFA  kwa mujibu wa kanuni na katiba

No comments:

Post a Comment